Mwananchi Digital
MTENDAJI ANUSURIKA KUWEKWA NDANI KUTOHUDHURIA KIKAO
- Title
- MTENDAJI ANUSURIKA KUWEKWA NDANI KUTOHUDHURIA KIKAO
- Runtime
- 4:36
- Date posted
- 1 hour ago
- Description
- Shinyanga. Mtendaji wa Kata ya Salawe, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, George Kuchibanda, amenusurika kuwekwa ndani baada ya Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro, kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi yanayomhusu mtendaji huyo, huku yeye mwenyewe akiwa hayupo katika hadhara hiyo kujibu malalamiko hayo.
Akizungumza leo Juni 14, 2026, katika ziara yake, Mtatiro ameagiza kuwa mtendaji huyo atafutwe haraka na aende kueleza kwa nini hajahudhuria mkutano huo wakati viongozi na watumishi wa Serikali ya wilaya wanatakiwa kuwepo. Amesema kama hatakuwa na majibu ya kuridhisha, awekwe ndani na wakutane naye kesho ili iwe funzo kwa wengine.
Malalamiko hayo yametolewa na mkazi wa Kijiji cha Songambele, Kata ya Salawe, Nkonya Mathias, akilalamika kuwa vijana wa kijiji hicho walifukuzwa na watu walioongozwa na mtendaji huyo katika stendi na kukatazwa kufanya biashara zao, jambo lililosababisha vurugu.
Mwananchi mwingine kutoka kata hiyo, Kanisio Maga...
- Title
- MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI MKOMBOZI MIGOGORO YA MIPAKA YA VIJIJI MSALALA
- Runtime
- 3:11
- Date posted
- 1 hour ago
- Description
- Zaidi ya wananchi 800 kutoka vijiji tisa vya Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, wanatarajiwa kunufaika na mpango wa matumizi ya ardhi, ikiwa ni jitihada za serikali kuhakikisha ardhi inatumika kuimarisha maendeleo ya jamii za vijijini.
Mwenyekiti wa kijiji cha Nata, kata ya Mwanase, Msalala, Charles Bulugu Juni 13, 2026, ameomba kuharakishwa mchakato wa upimaji wa maeneo ya kijiji ili kutambua mipaka ya kijiji hicho na kutatua mgogoro wa mpaka wa kijiji uliodumu kwa miaka 24.
Amesema “Tunashukuru huu mpango kutufikia, uharakishwe ili tuijue mipaka ya kijiji hiki na Mwakuhenga. Kuna eneo la kilimo hapa lakini sisi hatulimi na wale hawalimi kwa sababu kila mmoja anadhani ni kwake tangu mwaka 2002.”
Afisa mipango miji kutoka Tume ya Taifa ya Mpango wa matumizi ya ardhi Abdallah Magombana, amesema ukamilishaji wa shughuli hiyo, utakuwa suluhisho la migogoro ya muda mrefu, na wananchi wataendelea na shughuli zao za kiuchumi.
Ames...
- Title
- Ulikuwa unafahamu hili?
- Runtime
- 1:58
- Date posted
- 2 hours ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- NDOINYO ATAJA KITAKACHOMALIZA CHANGAMOTO NGORONGORO
- Runtime
- 17:52
- Date posted
- 2 hours ago
- Description
- Dodoma. Mbunge wa Ngorongoro, Yannick Ndoinyo amesema ushirikishwaji wa wananchi na kusikilizwa kwa maoni yao, ndiyo njia itakayomaliza changamoto zinazoikabili Ngorongoro, badala ya kutegemea uhamishaji wa watu pekee.
Ndoinyo amesema wananchi wengi wa wilaya hiyo hawataki kuhama kutoka maeneo yao ya asili, licha ya kuunga mkono juhudi za uhifadhi zinazoendelea katika eneo hilo. Amesisitiza kuwa kupata suluhu ya kudumu kuhusu hatima ya Ngorongoro kunahitaji mazungumzo ya wazi na kuwashirikisha wananchi katika maamuzi yanayohusu maisha yao na mustakabali wa eneo hilo.
Kauli hiyo imekuja wakati Ngorongoro ikiendelea kuwa kitovu cha mjadala wa kitaifa kuhusu namna bora ya kusawazisha masilahi ya uhifadhi na ustawi wa jamii zinazoishi ndani ya eneo la hifadhi.
Hoja za mbunge huyo zinafanana na yale yaliyobainishwa na tume iliyoundwa kuchunguza mchakato wa uhamishaji wa wananchi katika eneo hilo, ambayo ilieleza kuwa baadhi ya wananchi hawakuwa tayari ...
- Title
- HAYA NDIYO MAZISHI MZEE ONYANGO MAKABURI YA KONDO DAR
- Runtime
- 3:28
- Date posted
- 22 hours ago
- Description
- Hivi ndivyo mwili wa msanii mkongwe Issa Mohamed maarufu Mzee Onyango ulivyozikwa katika makamburi ya Kondo yaliyopo Ununio, Dar es Salaam leo Juni 13, 2026.
Mzee Onyango alifariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi, Juni 11, 2026, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mtoto wake, Joseph Issa, marehemu alifariki majira ya saa saba usiku baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa shinikizo la damu.
- Title
- TANZANIA YAFUNGUA RASMI SOKO LA NDIZI AFRIKA KUSINI
- Runtime
- 7:41
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- Tanzania imefungua rasmi soko la ndizi mbichi nchini Afrika Kusini baada ya kukamilika kwa majadiliano ya kitaalamu kuhusu matakwa ya afya ya mimea kati ya mamlaka husika za nchi hizo mbili.
Hatua hiyo imefikiwa kupitia mazungumzo kati ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) na Mamlaka ya Afya ya Mimea ya Afrika Kusini (NAPOZA), yaliyolenga kuridhiana kuhusu masharti ya afya ya mimea yanayoruhusu ndizi kutoka Tanzania kuingia katika soko la nchi hiyo.
Aidha, mauzo ya nje ya mazao ya kilimo ya Tanzania kwa sasa yanakadiriwa kufikia thamani ya takribani dola za Marekani bilioni 3.54 (sawa na zaidi ya shilingi trilioni 9.3 za Tanzania) kwa mwaka.
Kwa upande wa ndizi pekee, mauzo yake ya nje yanakadiriwa kuwa na thamani ya takribani dola za Marekani milioni 3.67 (zaidi ya shilingi bilioni 9.6 za Tanzania) kwa mwaka, yakipelekwa katika masoko mbalimbali yakiwemo Zambia, Malawi, Uganda na nchi za Umoja wa Ulaya (EU).
Ufun...
- Title
- RAIS MWINYI ALIVYOAGA MWILI WA MZEE ONYANGO
- Runtime
- 1:18
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi ni miongoni mwa waombolezaji waliojitokeza kuuaga mwili wa msanii mkongwe Issa Mohamed maarufu Mzee Onyango, Kawe jijini Dar es Salaam.
Mzee Onyango alifariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi, Juni 11, 2026, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mtoto wake, Joseph Issa, marehemu alifariki majira ya saa saba usiku baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa shinikizo la damu.
Marehemu Mzee Onyango anatarajiwa kuzikwa leo, Jumamosi, Juni 13, 2026, katika Makaburi ya Kondo yaliyopo Ununio, Dar es Salaam.
- Title
- MSAFARA ULIOBEBA MWILI WA MZEE ONYANGO UKIELEKEA MAKABURINI
- Runtime
- 4:10
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- Msanii Issa Mohamed ‘Mzee Onyango’ alifariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi, Juni 11, 2026, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mtoto wake, Joseph Issa, baba yake alifariki majira ya saa saba usiku baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa shinikizo la damu.
Marehemu Mzee Onyango anatarajiwa kuzikwa leo, Jumamosi, Juni 13, 2026, katika Makaburi ya Kondo yaliyopo Ununio, Dar es Salaam.
- Title
- MWANA FA AFICHUA YA MAREHEMU MZEE ONYANGO ENZI ZA UHAI WAKE
- Runtime
- 4:45
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'Mwana FA', amesema marehemu Issa Mohamed ‘Mzee Onyango’ alikuwa nyota mkubwa wa sanaa ya maigizo na ucheshi nchini, ambaye mchango wake ulihamasisha na kuvutia wasanii wengi kujikita katika tasnia ya sanaa kutokana na umahiri wake mkubwa wa kuigiza.
Msanii huyo mkongwe alifariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi, Juni 11, 2026, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mtoto wake, Joseph Issa, baba yake alifariki majira ya saa saba usiku baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa shinikizo la damu.
Marehemu Mzee Onyango anatarajiwa kuzikwa leo, Jumamosi, Juni 13, 2026, katika Makaburi ya Kondo yaliyopo Ununio, Dar es Salaam.
- Title
- MSIGWA: NILIVYOZIFANYA GWANDA ZA CHADEMA, NGUO ZA CCM ITABAKI ...
- Runtime
- 7:44
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alipoulizwa swali kuhusu alikozipeleka gwanda za Chadema mara baada ya kujiunga na CCM, na nguo za CCM baada ya kukikacha chama hicho na kurejea tena Chadema amesema hilo ni siri ya kambi.
Mchungaji Msigwa ambaye alikuwa mbunge wa Iringa Mjini kupitia Chadema kwa miaka 10 (2010-2020), alijiunga na CCM Juni 30, 2024 kabla ya kutangaza kurejea Chadema Mei 23, 2026 huku akitoa sababu kuu kwamba mauaji ya Oktoba 29, 2025 yalisukuma dhamira yake.
Mwananchi lilifanya mahojiano maalumu na Msigwa Jumanne Juni 2, 2026, jijini Dar es Salaam kuhusu uamuzi wake wa kuondoka CCM alikokaa takribani miaka miwili na kurejea Chadema ambako aliwahi kuwa mbunge na mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa.
Akizungumzia uamuzi wa kurejea Chadema, Mchungaji Msigwa amesema alitumia miezi sita kutafakari kuhusu uamuzi wake wa kuondoka CCM kutokana na mauaji ya wananchi yaliyofanyika wakati na baada ya uchaguz...
- Title
- #Live: RAIS SAMIA AKISHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA BENKI KUU YA TANZANIA, JNICC DAR ES SALAAM
- Runtime
- 2:10:16
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- RAIS SAMIA AKISHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA BENKI KUU YA TANZANIA, JNICC DAR ES SALAAM
- Title
- AKIBA YA DHAHABU BoT YAFIKIA TANI 27.5 ZENYE THAMANI YA SH10 TRILIONI
- Runtime
- 2:03
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema hadi kufikia Juni 10, 2026 ina akiba ya dhahabu ya tani 27.5 yenye thamani inayokadiriwa kufikia takribani Sh10 trilioni.
Hayo yamesemwa leo Ijumaa, Juni 12, 2026 na Gavana wa BoT, Emmanuel Tutuba, wakati wa Maadhimisho ya Miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania yanayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, ambapo Rais Samia Suluhu Hassan ndiye mgeni rasmi.
Tutuba amesema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Benki Kuu kuimarisha akiba ya taifa na kuongeza uthabiti wa uchumi wa nchi kupitia uwekezaji katika madini ya dhahabu kama mali salama ya kifedha.
“Mpaka kufikia Juni 10, 2026, Benki Kuu ina dhahabu tani 27.5 zenye thamani ya takribani Sh trilioni 10,” amesema Tutuba.
Aidha, BoT imekuwa ikiweka wazi mkakati wake wa kuongeza akiba ya dhahabu kwa kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wa ndani kupitia utaratibu rasmi wa kibenki. Hatua hiyo imekuwa ...
- Title
- RAIS SAMIA AZINDUA KITABU MAADHIMISHO YA BoT MIAKA 60, IPO ALBAMU YA NOTI
- Runtime
- 4:07
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Rais Samia Suluhu Hassan amezindua kitabu maalumu cha maadhimisho ya miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kinachojumuisha albamu ya matoleo mbalimbali ya noti zilizotumika nchini kuanzia mwaka 1966 hadi 2026.
Uzinduzi huo umefanyika leo, Juni 12, 2026, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), yanayofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam.
- Title
- BoT YAADHIMISHA MIAKA 60 IKIANZISHA KITENGO CHA AKILI UNDE
- Runtime
- 3:26
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeanzisha kitengo cha Akili Unde (AI) na ikisaini mikataba na vyuo vikuu sita nchini kwa lengo la kuimarisha uwezo wa kuchakata takwimu na kufanya maamuzi kwa kutumia taarifa zinazozalishwa na mifumo ya akili unde.
Hayo yameelezwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, ambaye amesema hatua hiyo imechochewa na ukuaji wa teknolojia za kifedha pamoja na ubunifu mpya unaoendelea kujitokeza duniani.
Ameongeza kuwa BoT imeendelea kuimarisha mifumo ya kudhibiti vihatarishi vinavyojitokeza katika huduma za malipo ya kidijitali, ili kuhakikisha teknolojia hizo zinaongeza ufanisi, kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha na kuimarisha uthabiti wa fedha bila kuleta uhararishaji wa fedha nchini.
Tutuba ameyasema hayo leo Ijumaa Juni 12, 2026 wakati wa Maadhimisho ya Miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yanayofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre jijini Dar ...
- Title
- Wananchi Vijibweni waibua kero za barabara, shule na migogoro ya ardhi mbele ya Chalamila
- Runtime
- 8:06
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Dar es Salaam.
Wananchi wa Mtaa wa Vijibweni, Wilaya ya Kigamboni, wameiomba Serikali kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili, zikiwemo ubovu wa barabara, uhaba wa madarasa na madawati shuleni pamoja na migogoro ya ardhi, wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ya kukagua miradi ya maendeleo katika eneo hilo.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika wakati wa ziara hiyo, wananchi walieleza kutoridhishwa na hali ya Barabara ya Soweto ambayo imeendelea kuwa kero kwa muda mrefu. Walidai kuwa matengenezo ya barabara hiyo yamekuwa yakifanyika kwa muda mfupi kila viongozi wanapotembelea eneo hilo, lakini husimama mara baada ya ziara hizo kukamilika.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Vijibweni, Mohamed Zigo, alisema juhudi zinazofanywa na wakandarasi zimekuwa za muda mfupi na kushindwa kutoa suluhisho la kudumu kwa changamoto ya miundombinu ya barabara. Alisema hali hiyo imeendelea kuathiri shughuli za kiuchumi na u...
- Title
- #Live: BAJETI KUU YA SERIKALI IKISOMWA BUNGENI DODOMA
- Runtime
- 1:52:05
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- #live HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA MIRADI YA NISHATI SAFI
- Runtime
- 22:50
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #live HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA
MIRADI YA NISHATI SAFI
- Title
- WANANCHI USANDA WALIA UHABA WA MAJI, RUWASA YAJIBU
- Runtime
- 3:20
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Shinyanga. Katika kliniki ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro inayohusiana na kusikiliza na kutatua kero za wananchi iliyoanza katika kata na Tarafa ya Samuye Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga, wananchi walia na changamoto ya maji huku wakiomba kuchimbiwa kisima kitakacho wasaidia kwa muda ambao watakuwa wakisubiri ujio wa maji ya ziwa Viktoria.
Akizungumza leo Juni 11, 2026 katika mkutano wa kusikiliza kero za wananchi, mkazi wa Kata ya Usanda George William Shija ameeleza kuwa kero hiyo imekuwa kwa muda mrefu na kwa muda mwingine wakazi wa mbali na mto huo wamekuwa wakiuziwa maji kutoka mto huohuo,
“Changamoto yangu ni maji ya mto tunayotumia si salama, nakero ya maji katika eneo hili imekuwepo kwa muda mrefu hatuna maji safi na salama, pia maji haya haya tunakunywa na kuchangia na mifugo, tunaomba angalau tuchimbiwe kisima cha maji kwa muda ambao tunasubiria kuunganishiwa maji ya ziwa Viktora” amesema Shija.
- Title
- #Live: BAJETI KUU YA SERIKALI IKISOMWA BUNGENI DODOMA
- Runtime
- 0:00
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- #live HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA MIRADI YA NISHATI SAFI
- Runtime
- 0:00
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #live HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA
MIRADI YA NISHATI SAFI
- Title
- #live HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA MIRADI YA NISHATI SAFI
- Runtime
- 2:26:03
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #live HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA
MIRADI YA NISHATI SAFI
- Title
- RC LINDI: WAKULIMA WA UFUTA HALMASHAURI YA MTAMA WALIPWE NDANI YA SIKU TATU
- Runtime
- 3:27
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Mkuu wa Mkoa wa Lindi (RC), Zainab Telack amewataka wanunuzi wa zao la ufuta kuhakikisha wakulima wanalipwa fedha zao ndani ya siku tatu baada ya kukamilika kwa mnada wa kwanza wa zao hilo uliofanyika kidijitali katika Halmashauri ya Mtama mkoani humo.
Akizungumza wakati wa mnada leo Juni 10, 2026 amesema mnada huo umehitimishwa kwa mafanikio baada ya ufuta wote uliokuwa umehifadhiwa kwenye maghala kuuzwa. akieleza kuwa bei ya juu ya ufuta ilikuwa Sh2,740 kwa kilo huku bei ya chini ikiwa Sh2,490 kwa kilo.
Aliongeza kuwa jumla ya kilo milioni 6.4 za ufuta zimeuzwa, huku wahasibu wa wanunuzi wakianza kuandaa ankara za malipo ili wakulima waweze kupata fedha zao kwa wakati.
Pia amezitaka benki na vyama vya ushirika kushughulikia kwa haraka changamoto za akaunti zitakazokataliwa ili kuhakikisha wakulima wote wanapokea malipo yao.
Aidha, amewaonya watu wanaochanganya ufuta na pumba au unga wa ufuta, akisisitiza kuwa hatua kali za kisheria ...
- Title
- WAKULIMA WA HALMASHAURI YA MTAMA LINDI WARIDHIA KUUZA UFUTA KWA SH2,740
- Runtime
- 9:35
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Wakulima wa ufuta wa Halmashauri ya Mtama mkoani Lindi wamekubaliana kuuza ufuta kwa bei ya Sh2,740 kwa kilo moja.
Katika mnada uliofanyika kwa Vyama Vikuu Viwili vya Ushirika vya Lindi, Mwambao na Arunali, zaidi ya kilo milioni 6.4 za ufuta ziliwasilishwa na zote kupata wanunuzi.
Akizungumza baada ya mnada huo leo Juni 10, 2026, Ofisa wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), Mahama Kadikilo amesema mnada umefanyika kwa mafanikio makubwa huku wakulima wakipata bei zinazoridhisha.
Amesema bei ya juu iliyopatikana ilikuwa Sh2,740 kwa kilo, huku bei ya chini ikiwa Sh2,490 kwa kilo, bei ambazo zote ni za mkulima.
“Kwa ujumla mnada wa leo umeenda vizuri. Ufuta wote uliowasilishwa uliuzwa na wakulima wamepata bei nzuri. Hii inaonesha kuwa soko la ufuta wa Lindi linaendelea kufanya vizuri,” amesema Kadikilo.
Aidha, amewataka wakulima kuendelea kuzingatia ubora wa mazao yao kwa kuhakikisha ufuta unasafishwa vizuri kabla ya kupelekwa...
- Title
- WANANCHI WAANIKA MATARAJIO YA BAJETI KUU YA SERIKALI
- Runtime
- 14:20
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Siku moja kabla ya kusomwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027, baadhi ya wananchi wameeleza maeneo wanayotamani yapewe kipaumbele, wakitoa mapendekezo yao katika sekta mbalimbali na kuitaka serikali kuelekeza nguvu zaidi kwenye maeneo hayo.
Mwananchi Digital leo Juni 10, 2026 imezungumza na wananchi kutoka mikoa mbalimbali nchini, ambao wamesema kuwa uboreshaji wa sekta hizo utasaidia kupunguza gharama za maisha, kuongeza fursa za kiuchumi na kuchochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja pamoja na taifa kwa ujumla.
Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 inatarajiwa kuwasilishwa bungeni kesho Alhamisi, Juni 11, 2026. Wananchi wameainisha matarajio yao wakisubiri kuona vipaumbele vitakavyopewa nafasi katika bajeti hiyo.
- Title
- BONI YAI: WANAOREJEA CHADEMA WASITARAJIE KUPATA VYEO HARAKA
- Runtime
- 4:34
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- Budget 2026/27: What Tanzanians, businesses and investors want to see
- Runtime
- 32:59
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- In this exclusive budget dialogue, KPMG Tanzania Tax Partners Fabiola Ssebuyoya and Samwel Esupu share their perspectives on the key tax and fiscal policy measures they believe should be prioritised in the 2026/27 national budget to support economic growth, attract investment, strengthen domestic revenue mobilisation, and accelerate Tanzania’s development agenda.
- Title
- EXCLUSIVE INTERVIEW PART 2 || MAGORI AFUNGUKA MAZITO MSIMBAZI
- Runtime
- 51:59
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- BONI YAI AWATAJA GEN Z ANGUKO LA MBOWE CHADEMA
- Runtime
- 7:52
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- #live BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA SITA
- Runtime
- 1:29:48
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #live BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA SITA
- Title
- ZAO LA UFUTA LINAVYOENDESHA MAISHA YA ASINA
- Runtime
- 10:18
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Kila punje ya ufuta anayovuna Asina Lutumbo wa Ngunichile, Nachingwea, hubeba hadithi ya maendeleo.
Ni punje zinazoweka chakula mezani. Ni punje zinazogharamia matibabu. Ni punje zinazowapeleka watoto na wajukuu shule. Ni punje zinazogeuka matumaini ya kesho.
Kwa mara ya kwanza msimu huu, Asina amepanda mbegu bora ya ufuta aina ya Lindi2002, iliyofanyiwa utafiti na kuzalishwa hapa nchini kupitia taasisi ya TARI na kusambazwa kwa wakulima na COPRA kwa wakulima kama Asina anayeuza ufuta wake kupitia minada ya kidijitali. Asina anaamini kuwa, kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo, mavuno yake yameongezeka na ndoto zake zitafanikiwa zaidi.
Kwa Asina, shamba si kipande cha ardhi tu. Ni benki yake, ni bima yake, ni chanzo cha ustawi wa familia yake.
𝗛𝗶𝗶 𝗻𝗱𝗶𝘆𝗼 𝗠𝗮𝗹𝗶 𝗦𝗵𝗮𝗺𝗯𝗮𝗻𝗶, 𝗮𝗺𝗯𝗮𝗽𝗼 𝗺𝗯𝗲𝗴𝘂 𝗯𝗼𝗿𝗮, 𝗺𝗮𝗮𝗿𝗶𝗳𝗮 𝗻𝗮 𝗷𝘂...
- Title
- #live BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TANO
- Runtime
- 1:30:38
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #live BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TANO
- Title
- MICHONGO CHANZO CHA FOLENI DAR ES SALAAM
- Runtime
- 16:16
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- MBEGU YA MAFANIKIO SAFARI YA WAKULIMA WA UFUTA NGUNICHILE
- Runtime
- 4:03
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- Hii ndiyo Mali Shambani! Kwa Seleman Mbaula wa Ngunichile, Nachingwea Mkoa wa Lindi.
Kilimo cha ufuta si zao tu bali ni biashara iliyomwezesha kubadili maisha ya familia yake. Ameweza kusomesha watoto wake na kujenga nyumba bora.
Kupitia matumizi ya mbegu bora ya ufuta aina ya Lindi zilizowezeshwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), ameongeza tija, mavuno na kipato.
Kutoka shambani hadi kwenye maisha bora huu ndio ushahidi kwamba kilimo biashara kinajenga mali, familia na mustakabali wa wadau kwenye mnyororo wa thamani wa zao hili la ufuta.
- Title
- #Live: MJADALA WA PPP KUHUSU MAGEUZI SEKTA YA AFYA NCHINI KUELEKEA DIRA 20250
- Runtime
- 2:00:40
- Date posted
- 8 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- UFUTA ULIVYOBEBA NDOTO YA SAFINA KUENDELEA NA MASOMO
- Runtime
- 5:00
- Date posted
- 8 days ago
- Description
- Mali Shambani ni zaidi ya mavuno, ni matumaini ya kesho. Katika kijiji cha Mipande, Masasi, familia ya Abdurahman Mohammed imewekeza kwenye kilimo cha ufuta kwa ndoto moja kubwa, kumpeleka binti yao Safina kujiunga na elimu ya juu.
Mwaka huu wamepanda mbegu bora ya ufuta aina ya Lindi 2002 iliyosambazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA).
Mbegu iliyotoa matumaini mapya na kuongeza matarajio ya kufanikisha ndoto za familia hii. Ukurasa mpya unatarajiwa kufunguliwa baada ya mavuno ya mbegu hii kuongezeka.
Kwa Safina, kila mmea wa ufuta unaoota shambani ni hatua moja karibu na ndoto yake ya kuwa Muhasibu katika chuo cha TIA. Kwa wazazi wake, ni tumaini la kuona juhudi za kilimo zikigeuka kuwa elimu, maendeleo na maisha bora.
Hii ndiyo nguvu ya Kilimo Biashara. Hii ndiyo Mali Shambani, ambapo shamba halizai mazao tu, linazalisha ndoto na fursa za maisha.
- Title
- #live: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU,KIKAO CHA 48 JUNI 5, 2026
- Runtime
- 1:50:21
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- DC Mpogolo ataka usimamizi wa sheria za mazingira Dar
- Runtime
- 13:12
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Mkuu wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo amezitaka Halmashauri za mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na taasisi za Udhibiti wa mazingira kusimamia Sheria kudumisha usafi wa mazingira katika mkoa huo.
Mpogolo ametoa kauli hiyo leo Juni 5,2026 wakati akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila wakati wa Maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani, ambayo kwa mkoa wa Dar es Salaam maadhimisho yamefanyika viwanja vya mnazi mmoja.
Amesema tatizo lililopo kwenye usimamizi wa mazingira ni uwajibikaji kwani tayari sheria zipo hazihitaji kutungwa zingine.
- Title
- KIHONGOSI AWAITA HECHE, LEMA NA BONI YAI KWENYE MDAHAL
- Runtime
- 2:56
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Arumeru. Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Kihongosi amesema anawataka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( Chadema) wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Bara), John Heche kwenye mdahalo.
Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Godbless Lema, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Boniface Jacob (Boni Yai).
Kihongosi ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Juni 5, 2026 alipokuwa akizungumza na wananchi katika viwanja vya Kanisa Katoliki Ngaramtoni, wilayani Arumeru, mkoani Arusha,ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani Arusha.
“Namtaka Heche aje hapa kushoto, Lema aje hapa kulia, Boni Yai asogee hapa na Sugu wa Mbeya akae hapa. Wote wawepo hao wanne, mimi niwe peke yangu halafu tuanze mdahalo,” amesema Kihongosi.
(Imeandikwa na Janeth Mushi)
- Title
- ZAIDI YA SH22.3 BILIONI KUBORESHA HUDUMA YA MAMA NA MTOTO, SHINYANGA
- Runtime
- 3:35
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Shinyanga. Mshauri elekezi wa mradi kutoka kampuni ya Volumetric Arch Consult Berno Batenamani ameeleza kuwa, mradi wa ujenzi wa jengo la mama na mtoto lenye ghorofa tano pamoja na maabara utaanza baada ya wiki mbili kuanzia leo, ambapo itakuwa Juni 19, 2026 na utatekelezwa kwa kipindi cha miaka miwili,
Akizungumza leo Juni 05, 2026 katika hafla fupi ya makabidhiano ya eneo la ujenzi katika Hospitali ya rufaa ya mkoa ya Shinyanga (Mwawaza) Batenamani ameeleza kuwa, mradi huo utagharimu kias cha Sh. 22.3 bilioni hadi kukamilika kwake na utakuwa na majengo mawili,
Naye mtekelezaji wa mradi huo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji kutoka kampuni ya Amar Builders Limited Vipul Naran amesema kuwa watafanya kazi kwa uaminifu na kwa kushirikiana na uongozi wa serikali ya mkoa na kumaliza ndani ya mkataba,
Aidha, Mganga mfawidhi kutoka Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga (Mwawaza) Daktari John Luzila ametoa shukrani kwa serikali kufikia hatua ya utekelezaji ...
- Title
- PARESSO AJITOLEA KUJENGA OFISI ZA CCM KARATU
- Runtime
- 8:02
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Arusha, Cecilia Paresso, ametangaza mpango wa kujenga na kukarabati ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kata mbalimbali za Wilaya ya Karatu ili kuimarisha shughuli za chama ngazi za chini.
Akizungumza Juni 4, 2026 mbele ya wanachama na viongozi wa CCM wilayani humo, Paresso amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha chama kinaendelea kuwa imara na kusogea karibu zaidi na wananchi.
“Jukumu la kujenga chama linapaswa kuwa letu sote bila kujali vyeo, dini wala makabila yetu,” amesema Paresso.
Amesema tayari ameandika barua rasmi kwa Kamati ya Siasa ya CCM kuhusu azma hiyo na kupokea ushirikiano wa kutosha wa utekelezaji wake.
Katika mkutano huo, Paresso pia amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi ya kuwaletea maendeleo Watanzania pamoja na kuimarisha chama hicho.
- Title
- HUDEFO WAZINDUA SHERIA NDOGO YA UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MIKOKO -LINDI
- Runtime
- 2:13
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- RAIS SAMIA AKISHIRIKI NA KUHUTUBIA JUKWAA LA 29 LA KIMATAIFA LA UCHUMI LA ST. PETERSBURG
- Runtime
- 39:12
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- RAIS SAMIA AKISHIRIKI NA KUHUTUBIA JUKWAA LA 29 LA KIMATAIFA LA UCHUMI LA ST. PETERSBURG
- Title
- BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TATU.
- Runtime
- 0:22
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TATU.
- Title
- MCHUNGAJI MSIGWA: WATAWALA WAKUBALI MAKOSA KUELEKEA MARIDHIANO YA KWELI
- Runtime
- 2:29
- Date posted
- 9 days ago
- Description
- Dar es Salaam. Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amesema njia pekee ya kuliponya Taifa na kulitoa katika hali ya sasa ni watawala kukubali makosa yao na kurejea kwenye misingi ya mazungumzo ya kweli na maridhiano.
Pia, amesema ili maridhiano yawe na maana, taasisi muhimu kama Bunge, Mahakama na Polisi ziachwe zifanye kazi zao kwa uhuru bila kuingiliwa na kwamba matatizo ya kisiasa yatatuliwe kisiasa na ya kiuchumi yatatuliwe kiuchumi.
Mchungaji Msigwa amebainisha hayo Juni 2, 2026 wakati wa mahojiano maalumu na Mwananchi, jijini Dar es Salaam, akizungumzia masuala mbalimbali ya kisiasa zikiwa zimepita wiki mbili tangu alipotangaza kurejea Chadema akitokea Chama cha Mapinduzi (CCM).
Msigwa ambaye alikuwa mbunge wa Iringa Mjini kupitia Chadema kwa miaka 10, alijiunga na CCM Juni 30, 2024 kabla ya kutangaza kurejea Chadema Mei 23, 2026 huku akitoa sababu kuu kwamba mauaji ya Oktoba 29, 2025 yalisukuma dham...
- Title
- BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TATU.
- Runtime
- 1:49:26
- Date posted
- 10 days ago
- Description
- BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TATU.
- Title
- Miezi 6 bila maji, kilio cha wakazi wa Tabata Darajani
- Runtime
- 10:34
- Date posted
- 10 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- EXCLUSIVE INTERVIEW PART 1 || MAGORI AFUNGUKA MAZITO MSIMBAZI
- Runtime
- 42:05
- Date posted
- 10 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- Mpaka wa Holili mguu sawa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola
- Runtime
- 3:17
- Date posted
- 10 days ago
- Description
- Wakati mamlaka zikiendelea kuongeza umakini na kuimarisha maandalizi ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini, hali katika mpaka wa Holili uliopo Wilaya ya Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro, imeelezwa kuwa shwari, huku kukiwa hakuna kisa chochote cha ugonjwa huo kilichoripotiwa hadi sasa.
Akizungumzia hali ya mpaka huo leo Juni 4, 2026 Kaimu Ofisa Mfawidhi afya mpaka wa Holili, Petro Mwani amesema hatua mbalimbali za tahadhari zinaendelea kuchukuliwa mpakani hapo ili kuzuia uwezekano wa ugonjwa huo kuingia nchini, huku wasafiri na wakazi wa maeneo ya mpaka huo wakihimizwa kuendelea kuzingatia miongozo ya afya inayotolewa na mamlaka husika.
Aidha, amesema kuwa, kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola unaoendelea katika mataifa jirani, maafisa wa afya mpakani hapo wamechukua tahadhari zote muhimu, ikiwemo kutoa elimu kwa makundi mbalimbali, wakiwemo wafanyakazi ambao hukutana na wasafiri wa aina tofauti wanaovuka mpaka huo.
- Title
- ALLY HAPI AMJIBU HECHE, LEMA MADAI YA UHURU WA KUTOA MAONI
- Runtime
- 2:59
- Date posted
- 10 days ago
- Description
- Katibu mkuu wa Jumuiya ya wazazi taifa Ally Hapi amejibu hoja za Makamu mwenyekiti taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Heche pamoja na mjumbe wa kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema, kuhusu kudai uhuru wa kutoa maoni huku wakiwa katika majukwaa na kuzungumza yote wanayoyataka.
Akizungumza leo Juni 04, 2026 baada ya mapokezi yaliyofanyika katika stendi ya soko kuu, Manispaa ya Shinyanga, huku akisema kuwa anashangaa uhuru wanaodai ni upi, huku akiongeza kuwa waache kuwasumbua wananchi na tone tone sababu wao ndio walikataa kushiriki uchaguzi ambao ungewasaidia kupata ruzuku,
“Wanapanda katika majukwaa na kuzungumza yote wanayotaka pamoja na kukejeli, Je, ni uhuru upi wanaouzungumzia kama wanapanda katika majukwaa na kukejeli” amesema Hapi.
- Title
- KUBADILISHA MIUONDOMBINU HUDUMA ZA UMMA
- Runtime
- 2:04:32
- Date posted
- 11 days ago
- Description
- KUBADILISHA MIUONDOMBINU HUDUMA ZA UMMA

