Azam TV
France 2-0 Morocco | Uchambuzi wa Mwinyi Zahera na Dkt. Licky baada ya mechi | AZAM TV
- Title
- France 2-0 Morocco | Uchambuzi wa Mwinyi Zahera na Dkt. Licky baada ya mechi | AZAM TV
- Runtime
- 5:16
- Date posted
- 22 minutes ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Je, nini kimeiponza Morocco? Huu hapa uchambuzi wa @lickyabdallah , Kocha Mwinyi Zahera na @james_samwel31
FT: France 2-0 Morocco
Inafuata Hispania vs Ubelgiji saa 4:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #FranceMorocco
- Title
- Uchambuzi wa vikosi na mifumo kuelekea mechi ya France vs Morocco | FIFA WC2026 | AZAM TV
- Runtime
- 8:30
- Date posted
- 2 hours ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Brian Tuka na Anthony Kimani katika uchambuzi wa mbinu na ufundi kwenye ‘pitch’, kwa kutazama vikosi vya timu zote mbili. Baada ya uchambuzi, wote wanatoa utabiri wao.
Je, Morocco wamejipangaje kumzuia Mbappe?
Tazama hapa.
Ni kuelekea mechi ya Ufaransa vs Morocco saa 5:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #FranceMorocco
- Title
- Kocha Mwinyi Zahera katika dawati la uchambuzi | France vs Morocco | FIFA WC2026 | AZAM TV
- Runtime
- 6:54
- Date posted
- 2 hours ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Je, hatua hii ingekuwa ni kitabu, jarada lake lingeandikwaje??
Msikilize @van_msumi wakati akilifungua dawati la uchambuzi, ambalo leo limejazwa pia na Kocha mwinyi Zahera.
Katika utangulizi wake, Kocha Zahera anasema “Wafaransa wanaona kombe hili ni lao”.
Zahera pia anaeleza sababu za timu ya taifa ya Congo DR kupanda kiwango ikilinganishwa na wakati ule yeye akiwa kocha wake msaidizi.
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #FranceMorocco
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Wasemavyo mashabiki Malawi kuelekea France vs Morocco | AZAM TV
- Runtime
- 3:18
- Date posted
- 2 hours ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Je, nani anakwenda nusu fainali kati ya Ufaransa na Morocco?
Kutoka Malawi, swali hili linajibiwa na mashabiki kwa Kiingereza na Chichewe.
Ni kuelekea mechi ya Ufaransa vs Morocco saa 5:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26
- Title
- Chiko Lawi alivyoufungua uchambuzi kuelekea mechi ya France vs Morocco | FIFA WC2026 | AZAM TV
- Runtime
- 5:24
- Date posted
- 2 hours ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Yalikuwa mataifa 48, kila moja likiwa na ndoto kubwa ya kulibeba Kombe la Dunia…. Lakini sasa yamebaki manane pekee, na leo wanaanza kuchujana kwenye hatua ya robo fainali.
@chikolawi akiwa na wachambuzi wake mahasimu kwa hoja…..Anthony Kimani na Brian Tuka wanatukaribisha kuuanza uchambuzi kuelekea robo fainali ya kwanza, Ufaransa vs Morocco.
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
- Title
- Mfumo mpya wa kusimamia ligi wazinduliwa, Rais Karia aeleza faida zake
- Runtime
- 7:14
- Date posted
- 7 hours ago
- Description
- Rais wa TFF, Wallace Karia ameshiriki katika uzinduzi wa mfumo mpya wa kidigitali wa kusimamia ligi, ambao pamoja na mambo mengine, utarahisisha kazi ya upangaji wa ratiba.
Akizungumza katika tuko hilo lililofanyika leo Julai 09, Dar es Salaam, Rais Karia amesema mfumo huo wa ufuatiliaji wa ligi, utasaidia pia kupunguza gharama kwa vilabu pamoja na kupunguza malalamiko ya wachezaji kuchoshwa na safari.
Haya hapa maelezo ya kutosha kuhusu mfumo huo…
#NBCPremierLeague
- Title
- Yanga SC yafika Azam Media na makombe yao kutoa shukrani kwa Washirika Wake.
- Runtime
- 28:17
- Date posted
- 13 hours ago
- Description
- YANGA NA MAKOMBE YAO: “Tupo hapa Azam leo kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa washirika wetu.”
Mkurugenzi wa Wanachama na Masoko wa Yanga SC, Ibrahim Samwel amesema ziara ya klabu hiyo katika ofisi za Azam Media leo Julai 9, 2026 imelenga kutoa shukrani kwa mshirika wao na kuonesha matokeo ya ushirikiano huo.
Ibrahim amesema Yanga SC haijafika Azam Media kwa ajili ya kuwashukuru mashabiki pekee, bali pia kuonesha namna ushirikiano kati ya pande hizo mbili ulivyozaa matunda.
- Title
- KIPYENGA CHA KOMBE LA DUNIA | Osman Kazi aingia na 'mgonjwa' studioni
- Runtime
- 2:26
- Date posted
- 14 hours ago
- Description
- KIPYENGA WC2026 | Namna gani pale…..?????
Timu ya #KipyengaChaKombeLaDunia imeingia na kiti mwendo studioni huku ving’ora vikirindima kila kona. Mwamuzi mstaafu wa soka @osmankazi1 ageuka daktari huku akimwacha mdomo wazi mtangazaji @katangaommy
Usikose kipindi hiki cha Kipyenga World Cup 2026 kila siku, saa tatu kabla ya mechi ya kwanza ya siku, kupitia maamuzi ya waamuzi kwenye mechi za Kombe la Dunia 2026.
#KipyengaWC2026 #KipyengaWorldCup2026
- Title
- Tanzania Prisons 0-0 Mbeya City | Highlights | NBC PL Play-off 08/07/2026
- Runtime
- 6:08
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- Timu ya Mbeya City imefanikiwa kusalia ligi kuu ya NBC baada ya kutoka suluhu dhid ya Tanzania Priosons, katika mchezo wa mtoano (mkondo wa pili) uliopigwa kwenye Dimba la Sokoine, Mbeya.
Katika mchezo wa mkondo wa kwanza, Mbeya City walishinda 2-0, hivyo wamefanikiwa kusalia kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-0.
- Title
- TFF Yatangaza VS Kuchukua nafasi ya VAR msimu ujao, Raisi wa TFF, Wallace Karia aeleza Sababu.
- Runtime
- 1:15:14
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- UCHAMBUZI: Mchambuzi wa soka, Michael Hyera ameeleza Mbwana Samatta ameacha alama ndani ya timu ya taifa ya Tanzania kutokana na kiwango chake kwa muda mrefu na kiwango thabiti alichokionesha akiwa nahodha wa 'Taifa Stars'.
Hyera amesema Samatta amekuwa na mwendelezo mzuri wa kiwango kwa miaka mingi, jambo lililomfanya kuwa mmoja wa wachezaji muhimu zaidi katika historia ya timu hiyo.Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema shirikisho hilo linatarajia kuanza kutumia mfumo wa VS kama mbadala wa Teknolojia ya Msaidizi wa Waamuzi kwa Njia ya Video (VAR), kuanzia msimu ujao wa mashindano.
Karia ameeleza kuwa uamuzi wa kuelekea kwenye mfumo wa VS umetokana na gharama zinazohusiana na ununuzi, uendeshaji na matengenezo ya VAR.
Amesema mfumo huo unaonekana kuwa suluhisho linaloendana zaidi na mazingira na uwezo wa kifedha wa soka la Tanzania kwa sasa.
- Title
- Rais Karia afunguka ratiba Muungano Cup, Mapinduzi Cup inavyoathiri ligi
- Runtime
- 3:11
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- AzRAIS KARIA “Lazima ligi iishe kabla ya AFCON”
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia, amesema kumekuwa na changamoto kwenye ratiba ya Ligi Kuu kutokana na kuathiriwa na mashindano ya Mapinduzi Cup na Muungano Cup, japo mashindano hayo ni muhimu.
Karia anasema wamepokea mapendekezo kuona namna gani mashindano hayo yafanyike.
Rais huyo wa TFF anasema mwakani kuna mashindano ya AFCON ambayo yataanza katikati ya mwezi Juni na inatakiwa ligi iishe mwezi mmoja kabla ili Timu ya Taifa ipate muda wa kujiandaa.
#Viwanjani
- Title
- Mbeya City 2-0 Tanzania Prisons | Highlights | Playoff 05/07/2026
- Runtime
- 8:16
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Kocha Moalin kuhusu Yanga SC na hali ya Pacome
- Runtime
- 2:39
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- YANGA SC: Baada ya kuichambua ‘come-back’ ya Argentina, Kocha Abdihamid Moalin anazungumza kuhusu Yanga akieleza ulivyokuwa msimu uliopita wa mashindano ambao wameondoka na ubingwa wa NBC Premier League…
Moalin anashukuru kwa mafanikio waliyopata, akisema kwa sasa anakwenda mapumziko, na akirejea ndipo atajua kuhusu mipango ya msimu ujao, lakini anaamini kwamba watarejea msimu ujao wakiwa imara zaidi.
Kocha Moalin pia anatoa taarifa kuhusu maendeleo ya kiungo wao Pacome Zouzoua huku akimtaja “Mama Samia”.
- Title
- Argentina 3-2 Egypt | Kocha Moalin aitofautisha na come-back ya Senegal | Uchambuzi (English)
- Runtime
- 6:21
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Je, kilichompa Misri leo ni sawa na kile kilichompata Senegal dhid ya Ubelgiji?
“…this one I think, it was a game of momentum, and we know the quality of Argentina”.
Mchambuzi mwalikwa wa leo, Kocha Abdihamid Moalin anatoa majibu ya kitaalamu hapa wakati dawati la kimombo likianza kuichambua ‘come-back’ ya mabingwa watetezi.
Moalini anasema kilichompata Senegal ni tofauti kabisa na hiki kilichompata Misri. Unajua tofauti ni nini?
msikilize hapa......
@felixsapao na @mr.bernardotieno_original nao wametoa maoni yao...
Je, wewe unaonaje.. ni kilekile au ni tofauti?
FT: Argentina 3-2 Egypt.
Inafuata Uswisi vs Colombia LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
- Title
- Argentina 3-2 Egypt | Je, Sub zimeiponza Egypt? | Uchambuzi wa Abissay na Dr. Leakey | FIFA WC 2026
- Runtime
- 6:24
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Je, ‘sub’ zilizofanywa na Misri ndiyo sababu ya kugeuziwa kibao na kupigwa?
Abissay Stephen anachambua akisema hiyo haikuwa sababu… na hapohapo Dkt. Leakey anasema tatizo ni ‘msosi’, (fitness) lakini pia anaitilia mashaka Argentina itakapokutana na England.
Je, wewe unasemaje?
FT: Argentina 3-2 Egypt.
Inafuata Uswisi vs Colombia LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
- Title
- Argentina 3-2 Egypt | Half-Time Analysis | FIFA World Cup 2026
- Runtime
- 3:57
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Uchambuzi baada ya kipindi cha kwanza; Je, nini kimeiweka salama Misri hadi sasa?
Hawa hapa Bernard Otieno, Felix Sapao na Kocha Abdihamid Moalin.
HT: Argentina 0-1 Egypt
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #ArgentinaEgypt
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Argentina vs Egypt | Kocha Moalin katika uchambuzi wa vikosi kabla ya mechi
- Runtime
- 7:47
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 | Kocha wa Yanga SC, Abdihamid Moallin katika uchambuzi wa vikosi na mifumo ya timu zote mbili, jinsi Messi atakavyokabiliana na Mo Salah.
Ni Argentina dhidi ya Misri.
LIVE #AzamSports2HD Kwa Kiswahili na #AzamSports4HD kwa Kiingereza.
#FIFAWorldCup2026 #WorldCup2026 #MechiZote104LiveAzamTV
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Wachambuzi wa soka wanasema ufalme wa soka kwa Brazil ndio basi tena
- Runtime
- 3:08
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 | “Mchezaji Bora wa wakati wote kwangu mimi ni Maradona”
Mchambuzi wa soka Felix Sapao ameonesha kutoungana na wale wanaobishana kuhusu ubora wa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, ambapo yeye anamtaja Maradona kuwa ndio bora kwake.
Bernard Otieno yeye anasema ufalme wa Brazil sasa baaasi.
LIVE #AzamSports2HD Kwa Kiswahili na #AzamSports4HD kwa Kiingereza.
#FIFAWorldCup2026 #WorldCup2026 #MechiZote104LiveAzamTV
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Hispania yamtupa nje Ureno, je itafika fainali? Msikilize Kocha Amani Josiah
- Runtime
- 2:13
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 | Tutegemee kuiona Hispania fainali? sikiliza majibu ya Kocha @amanijosiah23 akieleza tathmini yake ya dakika 90 za mchezo kati ya Ureno vs Hispania.
Mechi inayofuata ni USA vs Belgium saa 9:00 usiku.
LIVE #AzamSports2HD Kwa Kiswahili na #AzamSports4HD kwa Kiingereza.
#FIFAWorldCup2026 #WorldCup2026
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Imetosha kwa Ronaldo, Wachambuzi watoa heshima
- Runtime
- 1:08
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 | ''huwezi kuwa bora kwenye kila kitu'', ndivyo anavyosema @zakazakazi baada ya Ureno kupokea kichapo cha goli 1 kwa Hispania.
Tazama namna walivyoonesha heshima maalum kwa Cristiano Ronaldo.
LIVE #AzamSports2HD Kwa Kiswahili na #AzamSports4HD kwa Kiingereza.
#FIFAWorldCup2026 #WorldCup2026
- Title
- VIWANJANI: Pongezi kwa Simba SC na Yanga SC wakitumia Parade la ubingwa kuendeleza utani wa jadi.
- Runtime
- 45:19
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Wachambuzi wa soka, @akingamkono na @domayo wamepongeza namna klabu za Simba SC na Yanga SC wamekuwa wakitumia Parade la ubingwa kuendeleza utani wa jadi kwa namna inayoongeza ladha ya ushindani na kuwaburudisha mashabiki badala ya kuibua uhasama.
- Title
- Mashabiki wa Simba SC wakisheherekea ubingwa wa Kombe la Shirikisho la CRDB Bank 2025/26
- Runtime
- 1:24
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Mashabiki wa Simba SC ni shangwe tu leo..
Ilikua LIVE #AzamSports3HD
Kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama Parade hili na burudani nyingine.
#SimbaSC #Azamtvsports
- Title
- PARADE LA SIMBA SC: Mwali amefika Makao makuu ya Simba SC
- Runtime
- 3:42
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- PARADE LA SIMBA SC: Mwali amefika katika makao makuu ya Simba SC, Msimbazi na kituo kinachofuata ni Coco Beach.
Ilikua LIVE #AzamSports3HD
Kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama Parade hili na burudani nyingine.
#SimbaSC #Azamtvsports
- Title
- Magoli| Mbeya City 2 - 0 Tanzania Prison| NBC Premier League 05/07/2026
- Runtime
- 2:45
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- NBCPL| Mchezo wa mtoano wa ligi kuu NBC mkondo wa kwanza wa Mbeya City dhidi ya Tanzania Prison umemalizika, na haya ni magoli yote waliyofunga Mbeya City katika kipindi cha kwanza na cha pili, wafungaji ni Said Naushad na Hija Shamte.
Mchezo wa marudiano ni Julai 8, 2026 saa 10:00 jioni #AzamSports1HD ambapo Tanzania Prison watakuwa wenyeji wa mchezo.
FT: Mbeya City 2-0 Tanzania Prison.
#NBCPremierLeague #AzamSports1HD
- Title
- Canada 0-3 Morocco | Ulipokuwa uhatari wa Morocco (na Kocha Athuman Bemelengo)
- Runtime
- 2:06
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Kiufundi zaidi, hivi ndivyo yalivyokuwa makali ya Morocco hasa katika eneo lake la ushambuliaji.
Kocha Athuman Bemelengo, anamaliza namna hii…
FT’: Canada 0-3 Morocco
Inafuata Paraguay vs Ufaransa saa 6:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #CanadaMorocco
- Title
- Simba SC 1-0 Azam FC | Goli la Simba kwa Kiingereza | Fainali | CRDB Bank Fed. Cup 04/07/2026
- Runtime
- 1:41
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #CRDBBankFederationCupFinal Goli l Simba kwa ‘kimombo’ kama lilivyotangazwa na Chiko Lawi.
FT: Simba SC 1-0 Azam FC
Burudani zinaendelea LIVE #AzamSports1HD kwa Kiingereza na Kiswahili.
#KombeLaShirikishoLaCRDBBank #CRDBCup #FACup #MzizimaDerby #SimbaSC #AzamFC #SimbaAzam
- Title
- Canada 0-3 Morocco | Je, nani 'man of the match? Kocha Josiah anachambua
- Runtime
- 5:33
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Je, nani anastahili kuwa nyota wa mchezo huu? Sikia maoni na uchambuzi kutoka kwa Kocha Amani Josiah na James Samwel ambao pia wanachambua uwezo wa kocha wa Morocco, Mohamed Ouahbi
FT’: Canada 0-3 Morocco
Inafuata Paraguay vs Ufaransa saa 6:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #CanadaMorocco
- Title
- Canada 0-3 Morocco | Uchambuzi wa takwimu baada ya mechi (English) - FIFA World Cup 04/07/2026
- Runtime
- 3:21
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Sehemu ya uchambuzi baada ya game…
Felix Sapao anasema wanachokifanya Morocco si cha kubahatisha (fluke) bali ni matokeo ya mipango na mikakati waliyonayo tangu fainali zilizopita za Qatar….
Naye Bernard Otieno anasema kwa ubora walionao Morocco wanaweza kufika fainali (the last two).
Je, wewe unasemaje?
FT’: Canada 0-3 Morocco
Inafuata Paraguay vs Ufaransa saa 6:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
- Title
- Simba SC walivyokabidhiwa Kombe la Shirikisho la CRDB Bank 04/07/2026
- Runtime
- 5:14
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Simba SC imenyakua Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Azam FC bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Dimba la Gombani Pemba.
Goli pekee la ubingwa limefungwa Yahya Zayd ambaye amejifunga dakika ya 62.
Tazama sherehe za ubingwa, Simba wakikabidhiwa taji lao....
- Title
- Ahmed Ally atangaza ratiba ya 'paredi' la Simba SC baada ya ubingwa wa CRDB Bank Fed. Cup 04/07/2026
- Runtime
- 4:16
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- “.. pale Jangwani tutakuwa na kashughuli kadogo ka muda mfupi wa masaa matatu mpaka manne”
Baada ya ubingwa, Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amemwaga chozi huku akitangaza rasmi ratiba na ruti ya paredi la kusherehekea ubingwa huo.
FT: Simba SC 1-0 Azam FC
Enjoy Kombe la Dunia LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD .
#KombeLaShirikishoLaCRDBBank #CRDBCup #FACup #MzizimaDerby #SimbaSC #AzamFC #SimbaAzam #CRDBBankFederationCup
- Title
- Simba SC 1-0 Azam FC | Highlights | Fainali | CRDB Bank Federation Cup 04/07/2026
- Runtime
- 10:30
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Simba SC imenyakua Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Azam FC bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Dimba la Gombani Pemba.
Goli pekee la ubingwa limefungwa Yahya Zayd ambaye amejifunga dakika ya 62.
- Title
- Kadi nyekundu kwa Feitoto | Simba SC 1-0 Azam FC | Fainali | CRDB Bank Fed. Cup 04/07/2026
- Runtime
- 1:54
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Hili hapa tukio la kadi nyekundu 'red card', kwa kiungo wa Azam FC, Feisal Salum katika mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank uliopigwa kwenye Dimba la Gombani Pemba.
Katika mchezo huu, Simba imeibuka na ubingwa kwa ushindi wa bao 1-0 ambalo ni la kujifunga kupitia kwa kiungo Yahya Zayd.
- Title
- Goli la kujifunga | Simba SC 1-0 Azam FC | Fainali | CRDB Bank Fed. Cup 04/07/2026
- Runtime
- 1:48
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Simba SC imenyakua Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Azam FC bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Dimba la Gombani Pemba.
Goli pekee la ubingwa limefungwa Yahya Zayd ambaye amejifunga dakika ya 62.
- Title
- Wananchi wameitika kusheherekea ubingwa wa tano mfululizo kwa timu yao.
- Runtime
- 2:21
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Raisi wa Yanga SC, Injinia Hersi Said amesema wamelenga kuchukua ubingwa kwa msimu wa sita mfululizo
- Runtime
- 4:36
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- PARADE LA YANGA SC: "Tutaenda kuchukua Ubingwa msimu wa sita mfululizo..." Ni maneno ya Raisi wa Klabu ya Yanga SC, Injinia Hersi Said.
Iko LIVE #AzamSports3HD
- Title
- Vaibu la Wananchi kwenye Parade la ubingwa wa NBC PL kwa mara ya tano mfululizo.
- Runtime
- 3:26
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Kocha Ghana: Sasa ndiyo tunaanza Kombe la Dunia, aeleza atakachoifanya Colombia | FIFA WC 2026
- Runtime
- 4:57
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 : “The real Word Cup starts now”
Kocha Mkuu wa Ghana, Carlos Queiroz amesema sasa ndiyo wanaianza rasmi michuano ya Kombe la Dunia kwa kupambana na kuhakikisha wanavuka kuingia hatua ya 16 bora.
Akizungumza kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Colombia, Kocha Carlos amewataka wadau wasiihukumu timu hiyo kwa kiwango ilichokionesha katika mechi zilizopita, bali wawe na imani na uwezo wa wachezaji hao kuanzia hatua hii…
Kuhusu timu za Afrika kupoteza mechi za mtoano kwa magoli ya dakika za mwisho, Kocha Carlos amesema huo ndiyo utamu wenyewe wa soka na haina maana yoyote kama inavyotasfriwa na wengi, kwani goli linaweza kufungwa wakati wowote ndani ya dakika 90.
Kutoka Boston Marekani, huyu hapa Clive Kyazze na taarifa kamili.
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV
- Title
- Mashabiki Malawi wafunguka timu ya Afrika itakayoungana na Morocco 16 bora Kombe La Dunia 2026
- Runtime
- 3:25
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026: Kati ya Misri, Cape Verde ns Ghana, ni nani ataungana na Morocco kwenye hatua ya 16 bora?
Kutoka Blantyre Malawi, mashabiki wanatoa maoni yao, wakiitaja zaidi Misri. Lugha ya Chichewe pia imezungumza humu... sikiliza upate upate raha.
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Chiko Lawi afungua dawati la uchambuzi kwa story ya 'ndoa' (English)
- Runtime
- 8:27
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Ndivyo Chiko Lawi alivyoanza kwa simulizi ya kijana mmoja kutoka Kenya alivyoingia kwenye ndoa na mwanadada wa kitanzania miaka 50 iliyopia..
Lakini kubwa ni jinsi makocha wa timu za Afrika wanavyoachia ngazi baada ya kutupwa nje ya fainali za Kombe la Dunia.
Wachambuzi wake kama kawaida ni nyota wa zamani wa Harambee Stars, Anthony Kimani na Brian Tuka
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #AustraliaEgypy
- Title
- Prince Dube ameondoka Yanga SC rasmi baada ya misimu miwili, wachambuzi wanena.
- Runtime
- 50:20
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Uchambuzi | Deotraphe Kiungai amesema Dube kuondoka Yanga SC ni pigo kwa timu hiyo na kwenye ligi yetu kutokana na uwezo wake wa kuzunguka uwanjani, kukaa na mpira muda mrefu na kuwatengenezea nafasi wenzake pale timu inapomhitaji kufanya hivyo.
- Title
- "Tuna hamu nalo" - Kocha wa Simba SC kuelekea fainali ya CRDB Bank Fed. Cup dhidi ya Azam FC 2025/26
- Runtime
- 5:30
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #CRDBBankFederationCup “…tuna hamu kubwa ya kushinda kombe hili… ”
Kocha wa Simba, Steve Berker amesema kushinda Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kuna maana kubwa kwa klabu yao na mshabiki kiujumla kwakuwa hawajafikia hatua hiyo kwa muda mrefu..
Berker amesema wanahitaji kushinda kombe hili ili kujizawadia kwa kazi waliyoifanya kama timu pamoja na mashabiki
“…Ubingwa wa kombe hili utakuwa ni zawadi kwetu kwa juhudi ambazo tumezionesha kwa msimu mzima
Kuhusu maandalizi, Berker amesema kikosi kiko fiti, na wachezaji wote wakiwemo vijana na wakongwe, wote wako tayari kutoa mchango wao kwenye mchezo huo, ambao anaamini utakuwa mgumu.
Amesema utakuwa ni mchezo wa kimbinu zaidi kutokana na timu zote mbili kucheza soka la aina moja, akikumbushia kilichotokea kwenye mchezo wao wa mwisho kukutana.
Kwa niaba ya wachezaji wa Simba, beki Shomary Kapombe amesema fainali hiyo ni muhimu kwa ajili ya kutimiza...
- Title
- "Kombe tunalitaka" - Kocha Azam FC aeleza atakavyoivaa Simba Fainali ya CRDB Bank Fed. Cup 2025/26
- Runtime
- 3:39
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #CRDBBankFederationCup “…ubingwa tunautaka”
Kocha wa Azam FC, Florent Ibenge amesema kufika kwao fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank, kunamaanisha kwamba wanautaka ubingwa wa michuano hiyo huku akieleza umuhimu wa taji hilo kwao.
Mbele ya wanahabari kuelekea mchezo huo dhid ya Simba, Ibenge amesema wanatambua ubora wa wapinzani wao, lakini watafanya kila wanachokiweza dimbani ili kupata ushindi ushindi.
“…tutacheza mchezo wetu kama kawaida, tutaficha mpira na kusaka magoli…naamini Simba watakuwa bora na sisi pia tutakuwa bora, kwahiyo tutarajie mchezo mzuri”.
Naye kiungo wa timu hiyo Ashraf Kibeku kwa niaba ya wachezaji amesema wataingia dimbani kupambana na kupunguza makosa yaliyojitokeza kwenye michezo iliyopita, na ametoa ahadi kwa mashabiki.
Ni hapa katika Dimba la Gombani, Pemba kuelekea Fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank itakayopigwa kesho Julai 4, 2026.
Fainali ni saa 11:...
- Title
- Kombe la Dunia 2026: FIFA TSG Wazungumzia timu 48 na mafanikio ya timu za Afrika.
- Runtime
- 6:19
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Kutoka Boston Marekani, Clive Kyazze amezungumza na maafisa kutoka timu ya ufundi ya FIFA (FIFA TSG), Pablo Zabaleta (nyota wa zamani wa Argentina) na Pascal Zuberbuhler na Gilberto Silver kuhusu ongezeko la timu zinazoshiriki Kombe la Dunia kutoka 32 hadi 48, na faida zake kwa Afrika.
Magwiji hawa wanachambua pia kiwango cha timu za Afrika kwenye michuano ya mwaka huu akipongeza ongezeko la hamasa na ari ya upambanaji iliyoonekana….
Kwa upande wake Silva amepongeza ujio wa kanuni mpya zinazodhibiti upotevu wa muda uwanjani kama vile sekunde 10 za kufanya mabadiliko (substitution), na sekunde 5 za golikipa kuanzisha mpira.
Hii hapa taarifa yake…
- Title
- KOMBE LA DUNIA 2026 | Uchambuzi wa vikosi kuelekea mechi ya Hispania vs Austria
- Runtime
- 8:16
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026: Uchambuzi wa vikosi na mifumo kwa timu zote mbili kutoka kwa Anthony Kimani na Brian Tuka… !!
Ni Hispania vs Austria
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
- Title
- Fountain Gate FC 4-3 Singida BS | Highlights | NBC Premier League 30/06/2026
- Runtime
- 10:40
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- #NBCPL Tazama highlights, Singida BS akichezea kichapo, huku Mossi akipiga hattrick.
Magoli ya Fountain yamefungwa na Henry David, Obasi MacDonald na Hasheem Kindemile aliyefunga mawili.
Ni mech ya raundi ya 30 kuhitimisha msimu wa NBC Premier league 2025/26, kama ilivyopigwa kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Mambo yalikuwa hivi…
FT: Fountain Gate 4-3 Singida BS.
Ilikuwa LIVE #AzamTWO
#NBCPL #NBCPremierLeague #LigiKuuTanzania #ImenogaZaidi #FountainGateFC #SingidaBS #FountainGateSingidaBS
- Title
- Coastal union 2-1 Pamba Jiji | Highlights | NBC Premier League 30/06/2026
- Runtime
- 6:18
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- #NBCPL Tazama highlights, Wagosi wa Kaya wakijipigia mtu kwenye Dimba la Mkwakwani, Tanga.
Maabad Maulid Maabad ametia Kamba mbili na kuondoka na tuzo ya nyota wa mchezo, huku Pamba wakipata bao lao kupitia kwa Shassir Nahimana.
Hii ilikuwa ni mechi ya Raundi ya 30, kuhitimisha msimu wa Ligi Kuu ya NBC 2025/26
#NBCPL #NBCPremierLeague #LigiKuuTanzania #ImenogaZaidi #CoastalUnion #PambaJijiFC #CoastalUnionPambaJiji
- Title
- Yanga SC na maandalizi ya namna watakavyozunguka kusheherekea Ubingwa wa NBC PL.
- Runtime
- 1:06:04
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- Frank Domayo na Andrew Kingamkono wanachambua kwa kina kutamatika kwa Ligi Kuu ya NBC.
- Title
- NBCPL| Baraka mpenja alivyofunga matangazo ya mechi ya JKTS VS Yanga.
- Runtime
- 9:27
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- NBCPL: Hivi ndivyo Mwamba wa umalila, @baraka_mpenja alivyofunga matangazo ya mechi ya JKT dhidi ya Yanga SC ambao ndo mabingwa wa kombe la NBC Premier League msimu wa 2025/26 kwa mara ya tano mfululizo.
FT: JKT Tanzania 0-3 Yanga SC
✍ @miss_yustina1
#NBCPL #NBCPremierLeague #LigiKuuTanzania #ImenogaZaidi #JKTTanzania #YangaSC #JKTYanga
- Title
- Kombe la Dunia 2026 | Wachambuzi waumizwa na penati ya Ubelgiji kwa Senegal
- Runtime
- 2:18
- Date posted
- 8 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026: Wazee wa uchambuzi wa lugha ya kimombo leo ‘wamechafukwa’
Wameamua kulichambua kwa vitendo tukio la penati iliyoigharimu Senegal.
Ni @peterotaiofficial na wachambuzi wake Bernad Otieno na Felix Sapao.
Hewani muda huu ni Marekani dhidi ya Bosnia & Herzegovina.
Tuko LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #MarekaniBosnia
- Title
- Ubishi kuhusu kiwango cha England dhidi Congo DR (2-1) | Kombe la Dunia 2026 (English)
- Runtime
- 8:51
- Date posted
- 8 days ago
- Description
- #KombeLaDunia2026 Hii ligi ya studio kati ya Brian Tuka na Anthony Kimani naona imezidi kuwa ngumu…..!!
Tuka amefika mbali zaidi, na sasa anabishana na takwimu za mechi, akipinga England kupewa sifa kihivyo….
Anasema krosi nyingi walizopiga kusaka bao hazikuwa za kimipango, bali ni za kuchanganyikiwa…
Mwishoni kabisa Chiko anamnyooshea mikono na kusema endapo akipata kesi kwa mkewe inayohitaji kubishana, kazi hiyo hiyo atampa Brian Tuka.
Hebu tazama hii….!!!
FT: England 2-1 Congo DR
Inafuata Ubelgiji vs Senegal saa 5:00 usiku LIVE #AzamSports2HD na #AzamSports4HD
#FWC26 #FIFAWorldCup #WeAre26 #FIFAWorldCup2026NyumbaniAzamTV #MechiZote104LiveAzamTV #EnglandCongoDR

