Azam TV
Kocha wa Yanga Manqoba ameanza kwa kumchambua Kocha Minziro kuelekea mechi ya Fountain Gate
- Title
- Kocha wa Yanga Manqoba ameanza kwa kumchambua Kocha Minziro kuelekea mechi ya Fountain Gate
- Runtime
- 8:42
- Date posted
- 17 hours ago
- Description
- FOUNTAIN GATE vs YANGA SC: Utaratibu ni uleule kwa Kocha Manqoba Mngqithi wa Yanga SC, ambaye amekuwa akichambua vikosi vya wapinzani wake kwa kutaja majina ya mchezaji mmoja baada ya mwingine.
Leo ameanza na Kocha Fred Felix ‘Minziro’ ambaye anasema ni legend wa Yanga na bila shaka anajua ari na utaratibu wa klabu hiyo.
Manqoba ametaja mpaka mfumo ambao Fountain Gate hutumia.
Kwa upande wake mchezaji Juma Issa Abushiri ‘Chuga’ ameelezea namna alivyopokea kile ambacho kilizungumzwa na kocha wake baada ya mechi dhidi ya JKT Tanzania.
Mechi ni kesho Agosti 31, 2026, saa 10:00 jioni LIVE #AzamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi
- Title
- Kocha Fountain Gate akiri ubora wa Yanga, ajipanga kukabiliana nao
- Runtime
- 2:27
- Date posted
- 18 hours ago
- Description
- FOUNTAIN GATE vs YANGA SC: “Hatuna maingizo mapya”
Kocha wa Fountain Gate, Fred Felix ‘Minziro’ anasema ni kweli wanakutana na timu inayocheza vizuri na kushambulia kwa kasi lakini wao wataingia na mbinu ya kupambana nao ili kupunguza kasi yao.
Kocha huyo anasema ataendelea kuwatumia wachezaji alionao kwasababu timu yake haina wachezaji wapya kutokana na changamoto za usajili.
Kwa upande wake mchezaji Obasi Macdonald, anasema wao wapo tayari kwa mechi ya kesho na wanajua aina ya timu wanayokwenda kukutana nayo.
Mechi ni kesho Agosti 31, 2026, saa 10:00 jioni LIVE #AzamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi
- Title
- Kocha Katwila wa Geita Gold asema wapo tayari kuivaa Simba
- Runtime
- 1:07
- Date posted
- 20 hours ago
- Description
- SIMBA vs GEITA GOLD: “Wana wachezaji wanaoweza kuamua mechi”
Kocha Zuberi Katwila wa Geita Gold anasema wapinzani wao wana wachezaji wenye uwezo mkubwa na wao wamejipanga kukabiliana nao.
Kwa upande wake nahodha wa kikosi hicho Yusufu Mhilu anasema wao wachezaji wanajua kuwa kesho Agosti 31, 2026 wanakwenda kucheza na timu inayotafuta ubingwa na wao wamejipanga kuikabili.
Mechi ni saa 12:30 usiku LIVE #AzamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi
- Title
- Kocha Barker wa Simba alia na majeruhi, adhabu kuelekea mechi ya Geita Gold
- Runtime
- 1:53
- Date posted
- 20 hours ago
- Description
- SIMBA vs GEITA GOLD: “Maandalizi yanaendelea vema”
Kocha wa Simba SC, Steve Barker anasema kuna changamoto ya majeruhi katika safu yake ya ulinzi lakini pia wapo baadhi ya wachezaji tegemeo hawatopatikana kuelekea mchezo wa kesho wa NBC Premier League dhidi ya wageni wao Geita Gold.
Kwa upande wake mchezaji Hussein Daud Semfuko anasema wanajua umuhimu wa mchezo wa kesho na wamejiandaa kuzipambania alama tatu.
Mechi ni saa 12:30 usiku LIVE #AzamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi
- Title
- JKT Tanzania 2-1 Namungo | Magoli | NBC Premier League - 29/08/2026
- Runtime
- 3:30
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- #NBCPL: Tazama magoli yote matatu yaliyofungwa kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya JKT Tanzania dhidi ya Namungo FC.
Magoli ya JKT Tanzania yamefungwa na Paul Peter Kasunda na Said Mkopi huku goli la Namungo likiwekwa nyavuni na Hassan Wahabi amabaye amejifunga.
FT: JKT Tanzania 2-1 Namungo FC
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #JKTTanzania #Namungo
- Title
- Singida BS 4-2 Polisi Tanzania | Highlights | NBC Premier League - 29/08/2026
- Runtime
- 10:25
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- #NBCPL: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya Singida BS dhidi ya Polisi Tanzania katika dimba la Airtel mkoani Singida.
Chuma sita zilizofungwa kwenye mchezo kati ya Singida BS dhidi ya Polisi Tanzania.
Ilianza Polisi kupitia Baraka Michael na goli lao la pili lilifungwa na Ibrahim Ame.
Wenyeji Singida BS wakafungua karamu ya magoli kupitia Jonathan Sowah, kisha James Mwashinga, Shekhan Ibrahim na baadae Jeancy Mboma akaweka goli la nne.
FT: Singida BS 4-2 Polisi Tanzania
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #SingidaBS #PolisiTanzania
- Title
- TRA United 0-1 Dodoma Jiji | Highlights | NBC Premier League - 29/08/2026
- Runtime
- 8:54
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- #NBCPL: Matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya TRA United dhidi ya Dodoma Jiji.
Mechi imepigwa katika dimba la Sheikh Amri Abeid.
Mfungaji ni William Edgar.
FT: TRA United 0-1 Dodoma Jiji
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #TRAUnited #DodomaJiji
- Title
- Singida BS 4-2 Polisi Tanzania | Magoli | NBC Premier League - 29/08/2026
- Runtime
- 6:40
- Date posted
- 1 day ago
- Description
- #NBCPL: Chuma sita zilizofungwa kwenye mchezo kati ya Singida BS dhidi ya Polisi Tanzania.
Ilianza Polisi kupitia Baraka Michael na goli lao la pili lilifungwa na Ibrahim Ame.
Wenyeji Singida BS wakafungua karamu ya magoli kupitia Jonathan Sowah, kisha James Mwashinga, Shekhan Ibrahim na baadae Jeancy Mboma akaweka goli la nne.
FT: Singida BS 4-2 Polisi Tanzania
Saa 3:00 usiku ni JKT Tanzania dhidi ya Namungo FC LIVE #AzamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #SingidaBS #PolisiTanzania
- Title
- TRA United 0-1 Dodoma Jiji | Uzuri wa jiji la Arusha - 29/08/2026
- Runtime
- 2:05
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #NBCPL: Tazama uzuri wa maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha na shughuli zinazofanyika hasa utalii.
Mtangazaji @hinjojr ndiye msimulizi wako wakati akiifungua mechi ya NBC Premier League kati ya TRA United dhidi ya Dodoma Jiji.
FT: TRA United 0-1 Dodoma Jiji
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #TRAUnited #DodomaJiji
- Title
- TRA United 0-1 Dodoma Jiji | Goli | NBC Premier League - 29/08/2026
- Runtime
- 1:00
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #NBCPL: Goli lililoilaza TRA United na kuiruhusu Dodoma Jiji ikiondoka na alama tatu.
Mfungaji ni William Edgar.
FT: TRA United 0-1 Dodoma Jiji
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #TRAUnited #DodomaJiji
- Title
- TRA United 0-1 Dodoma Jiji | Kadi nyekundu kwa Kelvin Kijili - 29/08/2026
- Runtime
- 2:13
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- #NBCPL: Matukio mawili yaliyosababisha kadi mbili za njano kwa Kelvin Kijili wa TRA United.
Mfungaji ni William Edgar.
FT: TRA United 0-1 Dodoma Jiji
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidI #TRAUnited #DodomaJiji
- Title
- KURASA ZA MWISHO | 29/08/2026.
- Runtime
- 57:31
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- ''hata baada ya AFCON tutabaki na miundombinu mizuri'',
Wachambuzi wa Soka, Khatimu Naheka, Philip Nkini, Jabir Juma na Charles Abel wakieleza maboresho ya viwanja na miundombinu yanayoendelea kufanyika kuelekea AFCON 2027.
Azam TV
- Title
- Yanga SC 2-0 Pamba Jiji FC | Highlights | NBC PL 28/08/2026
- Runtime
- 3:36
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Cheikh Ibrahima Toure amefunga moja na kutoa assist moja, Yanga ikishinda 2-0 dhidi ya Pamba Jiji, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam.
Mfungaji wa goli la kwanza alikuwa ni Maxi Nzengeli..
- Title
- Magoli | Yanga SC 2-0 Pamba Jiji | NBC Premier League 28/08/2026
- Runtime
- 2:46
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Cheikh Ibrahima Toure amefunga moja na kutoa assist moja, Yanga ikishinda 2-0 dhidi ya Pamba Jiji, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam.
Mfungaji wa goli la kwanza alikuwa ni Maxi Nzengeli..
- Title
- Geita Gold FC 2-2 Azam FC | Highlights | NBC Premier League 28/08/2026
- Runtime
- 3:24
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Ni sare ya maajabu kwenye Dimba la Bukombe, Ushirombo, mkoani Geita, Azam FC wakichomolewa dakika za jiooooooni.
Azam wametangulia kwa penati kupitia kwa Abdul Suleiman Sopu, lakini wakachomoa kupitia kwa Obrey Chirwa...
Kunako dakika za majeruhi, Azam wakafunga kupitia kwa Himid Mao, lakini dakika mbili baadaye wakachomoa kupitia kwa Martin Kigi.
Hii ni Ligi Kuuya NBC.
- Title
- Magoli | Geita Gold FC 2-2 Azam FC | NBC Premier League 28/08/2026
- Runtime
- 6:13
- Date posted
- 2 days ago
- Description
- Ni sare ya maajabu kwenye Dimba la Bukombe, Ushirombo, mkoani Geita, Azam FC wakichomolewa dakika za jiooooooni.
Azam wametangulia kwa penati kupitia kwa Abdul Suleiman Sopu, lakini wakachomoa kupitia kwa Obrey Chirwa...
Kunako dakika za majeruhi, Azam wakafunga kupitia kwa Himid Mao, lakini dakika mbili baadaye wakachomoa kupitia kwa Martin Kigi.
Hii ni Ligi Kuuya NBC.
- Title
- Fountain Gate 0-2 Mbeya City | Highlights | NBC PL 28/08/2026
- Runtime
- 8:14
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #NBCPL ‘Majanga’ ya super sub, Oscar Mwajanga akitokea benchi na kuchapa chuma mbili yeye peke yake…!!!
FT: Fountain Gate 0-2 Mbeya City
Hii ni Ligi Kuu ya NBC, mchezo ukipigwa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
- Title
- Magoli ya Mwajanga | Fountain Gate 0-2 Mbeya City | NBC Premier League 28/08/2026
- Runtime
- 2:11
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- #NBCPL ‘Majanga’ ya super sub, Oscar Mwajanga akitokea benchi na kuchapa chuma mbili yeye peke yake…!!!
FT: Fountain Gate 0-2 Mbeya City
Hii ni Ligi Kuu ya NBC, mchezo ukipigwa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
- Title
- Simba SC TV | Wiki hii imeangazia matukio muhimu, kabla na baada ya mchezo dhidi ya Singida BS.
- Runtime
- 26:12
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- MSHIKEMSHIKE | 28/08/2026.
- Runtime
- 45:29
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Simba SC Yaanza kwa ushindi nyumbani dhidi ya Wanamangushi.
- Runtime
- 33:39
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Mchambuzi wa soka, George Job amesema mashabiki wa Simba SC wanapaswa kuelewa kuwa lengo kuu lilikuwa kupata alama tatu, badala ya kuangalia idadi kubwa ya magoli.
Amesisitiza umuhimu wa kumheshimu kila mpinzani na kuthamini ushindi uliopatikana.
Azam TV
- Title
- NBCPL: Mwamba wa Umalila alivyoanza na simulizi bomba; Simba vs Coastal Union Meja Jenerali Isamuhyo
- Runtime
- 3:00
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Simba SC 1-0 Coastal Union | Highlights | NBC Premier League 27/08/2026
- Runtime
- 9:35
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Beki Ismail Toure amefunga goli pekee lililoipa Simba alama tatu muhimu dhidi ya Coastal Union, mchezo wa ligi kuu ya NBC, uliopigwa kwenye Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam.
- Title
- Goli pekee la Simba SC dhidi ya Coastal Union (1-0) | NBC Premier League 27/08/2026
- Runtime
- 1:49
- Date posted
- 3 days ago
- Description
- Beki Ismail Toure amefunga goli pekee lililoipa Simba alama tatu muhimu dhidi ya Coastal Union, mchezo wa ligi kuu ya NBC, uliopigwa kwenye Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam.
Tazama goli...
- Title
- Mashujaa FC 2-1 Kagera Sugar | Highlights | NBC Premier League 27/08/2026
- Runtime
- 4:06
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Mashujaa FC wamefanya 'come-back' na kushinda 2-1 dhidi ya Kagera Sugar waliokuwa wametangulia kwa goli la Mudathir Abdulla Said.
Magoli ya Mashujaa yamefungwa ndani ya dakika ya saba, wafungaji wakiwa ni Mishamo Daud na Haroun Lyawatwa ..
Mechi imepigwa kwenye Dimba la Lake Tanganyika, Kigoma.
- Title
- Magoli | Mashujaa FC 2-1 Kagera Sugar | NBC Premier League 27/08/2026
- Runtime
- 4:26
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Mashujaa FC wamefanya 'come-back' na kushinda 2-1 dhidi ya Kagera Sugar waliokuwa wametangulia kwa goli la Mudathir Abdulla Said.
Magoli ya Mashujaa yamefungwa ndani ya dakika ya saba, wafungaji wakiwa ni Mishamo Daud na Haroun Lyawatwa ..
Mechi imepigwa kwenye Dimba la Lake Tanganyika, Kigoma.
- Title
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI | Doumbia kuanza kufunga dhidi ya Coastal...????
- Runtime
- 10:51
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- VIWANJANI: Simba SC yapewa nafasi kubwa dhidi ya Coastal Union.
- Runtime
- 22:54
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Mchambuzi wa soka, Khalid Chukuchuku anaamini Simba SC ina nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa leo, akitaja faida ya kucheza nyumbani na uimara wa kikosi cha Simba kwa sasa.
Mtazamo huo umeungwa mkono na wachambuzi wa soka Ramadhani Mbwaduke na Frank Domayo ambao wanaona mazingira ya mchezo yanaipa Simba SC nafasi ya kupata alama tatu.
Azam TV
- Title
- MSHIKEMSHIKE | 26/08/2026.
- Runtime
- 35:17
- Date posted
- 4 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Je, unapajua 'Mwisho wa Reli'? Ni hapa....
- Runtime
- 3:19
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- KUTOKA KIGOMA | “..Mambo kwa ushahidi”
Kuna ule msemo wa ‘Mwisho wa Reli Kigoma’; Je umeshawahi kuwaza hapo mwisho wa reli penyewe panafananaje?
Timu yetu ya Azam Sports ambayo ipo Kigoma kwaajili ya mchezo wa Ligi kuu ya NBC kati ya Mashujaa FC dhidi ya Kagera Sugar inakuletea simulizi fupi ya mwisho wa reli kwa ushahidi….
Huyu hapa @wastara24 akituoneshe ‘Mwisho wa Reli’.
Mechi inapigwa kesho Agosti 27 saa 10:00 jioni LIVE #azamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi #MashujaaFC #KageraSugar
- Title
- Coastal Union yajipanga kuitibua Simba SC.
- Runtime
- 1:37
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- SIMBA SC vs COASTAL UNION: Kocha wa Coastal Union, Fikiri Elias amesema benchi lake la ufundi limefanya kazi ya kutosha kuzisoma mbinu za Kocha wa Simba SC, Steve Barker kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu ya NBC.
Fikiri amesema wamejiandaa vyema kukabiliana na mipango ya Simba SC na wanaingia uwanjani wakiwa na lengo la kuondoka na alama zote tatu.
Azam TV
- Title
- VIWANJANI: Mjadala timu sita ambazo hazijapata ushindi mpaka sasa NBC Premier League.
- Runtime
- 38:24
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Wachambuzi wa soka wamezungumzia mwenendo wa timu sita ambazo hadi sasa hazijapata ushindi wa alama tatu katika Ligi Kuu ya NBC.
Miongoni mwa timu hizo ni Kagera Sugar, ambayo imekuwa ikipambana kusaka ushindi katika mwendelezo wa ligi chini ya Kocha Juma Kaseja.
Mchambuzi wa soka, Amri Kiemba amesema sasa ni wakati kwa kocha Kaseja kuangalia namna bora ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji na kuongeza kasi pamoja na ufanisi wa kupata mabao, ili Kagera Sugar iweze kuanza kuvuna alama tatu dhidi ya wapinzani wake.
Azam TV
- Title
- Simba vs Coastal Union: Matola aweka wazi maandalizi ya kikosi kuelekea mchezo wao na Coastal Union.
- Runtime
- 1:47
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola akizungumzia maandalizi ya kikosi chake kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Coastal Union.
Matola amesema mpinzani wao amekuwa hana matokeo mazuri lakini anaonesha mchezo mzuri jambo ambalo linaonesha mechi itakuwa ngumu.
Azam TV
- Title
- VIWANJANI: Namungo haijawa imara.
- Runtime
- 28:05
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Mchambuzi wa soka, George Job amesema Namungo ya sasa imepoteza baadhi ya misingi iliyoiwezesha kufika Ligi Kuu, akitaja mabadiliko ya bajeti, falsafa ya usajili na mambo mengine ya msingi kuwa miongoni mwa sababu zinazofanya timu hiyo ionekane tofauti na ile iliyopanda daraja.
Azam TV
- Title
- Dodoma Jiji 0-1 Polisi Tanzania | Highlights | NBC Premier League 25/08/2026
- Runtime
- 6:41
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #NBCPL Tazama highlights, Anuary Jabir akiifunga timu yake ya zamani na kushangilia hadi ‘kuweka kando’ jezi yake: Je, ina maana gani?
FT: Dodoma Jiji 0-1 Polisi Tanzania.
Hii ni mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara ikipigwa Jamhuri Stadium, Dodoma.
- Title
- Goli la Anuary Jabir | Dodoma Jiji 0-1 Polisi Tanzania | NBC Premier League 25/08/2026
- Runtime
- 1:25
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- #NBCPL Tazama goli la Anuary Jabir akiifunga timu yake ya zamani na kushangilia hadi ‘kuweka kando’ jezi yake: Je, ina maana gani?
FT: Dodoma Jiji 0-1 Polisi Tanzania.
Hii ni mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara ikipigwa Jamhuri Stadium, Dodoma.
- Title
- Namungo FC 1-0 Fountain Gate FC | Highlights | NBC Premier League 25/08/2026
- Runtime
- 4:07
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Goli pekee kutoka kwa Herbert Lukindo limeipa alama tatu muhimu Namungo FC, kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Fountain Gate FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Majaliwa Stadium, Ruangwa Lindi.
- Title
- Goli pekee | Namungo FC 1-0 Fountain Gate FC | NBC Premier League 25/08/2026
- Runtime
- 1:16
- Date posted
- 5 days ago
- Description
- Goli pekee kutoka kwa Herbert Lukindo limeipa alama tatu muhimu Namungo FC, kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Fountain Gate FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Majaliwa Stadium, Ruangwa Lindi.
Hili hapa goli
- Title
- VIWANJANI : Coastal Union wagawana alama na TRA United.
- Runtime
- 33:37
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Wachambuzi wafunguka mitazamo yao baada ya Coastal Union kushindwa kubakisha alama zote tatu mbele ya TRA United.
Azam TV
- Title
- VIWANJANI : Yanga yaendeleza mwendo kuzinyakua alama tatu! kipigo cha magoli 4-0 kwa JKT Tanzania.
- Runtime
- 38:22
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Mchambuzi wa soka Lilian Mukulu amesema mchakato wa Shalulile kulitafuta na kulifunga goli katika mchezo wao wa NBC Premier League ulikuwa bora, akisisitiza namna Yanga wanavyotumia kasi na nguvu ya mashambulizi yao.
Azam TV
- Title
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI | JKT Tanzania yasema kila timu itakutana na Yanga
- Runtime
- 15:07
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI: “Uzuri kila mtu atacheza nao hawa jamaa” JKT Tanzania wanasema kila timu itakutana na Yanga.
Ni #Zilizobamba mitandaoni kupitia kipindi cha viwanjani.
#Zilizobamba #Viwanjani
- Title
- Coastal Union 1-1 TRA United | Highlights | NBC Premier League 24/08/2026
- Runtime
- 7:09
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #NBCPL Ni sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.. mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliowakutanisha wenyeji Coastal Union dhidi ya TRA United.
Aliyetangulia kufunga alikuwa ni Ani Elijah kabla ya Shiza Kichuya kuchomoa kwa tikitaka fulani hivi.
- Title
- Magoli | Coastal Union 1-1 TRA United | NBC Premier League 24/08/2026
- Runtime
- 2:20
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Ni sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.. mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliowakutanisha wenyeji Coastal Union dhidi ya TRA United.
Aliyetangulia kufunga alikuwa ni Ani Elijah kabla ya Shiza Kichuya kuchomoa kwa tikitaka fulani hivi.
Haya hapa magoli yote...
- Title
- Kocha Yanga hajaridhika na ushindi wa 4-0 dhidi ya JKT Tanzania (neno la makocha baada ya mechi)
- Runtime
- 4:31
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- #NBCPL Kocha wa Yanga Manqoba Mngqithi ameeleza kutoridhishwa na ushindi wa 4-0 alioupata leo dhidi JKT Tanzania, akisema walistahili kupata mabao mengi zaidi.
Kocha Manqoba amesema bado wana kazi ya kufanya na kwamba anashukuru kuona kikosi chake kinaimarika siku hadi siku...
Kwa upande wake Kocha wa JKT Tanzania, Ahmad Ally anaeleza kilichomfelisha kwenye mchezo wa leo, kubwa ikiwa ni wachezaji wake kupoteza umakini…
Kocha Ahmad pia anaeleza jinsi atakavyoirekebisha timu yake kiufundi, akisema “bado tuna kazi ya kufanya”.
- Title
- Yanga SC 4-0 JKT Tanzania | Highlights | NBC Premier League 24/08/2026
- Runtime
- 12:42
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Yanga SC imeishusia kichapo kizito JKT Tanzania cha mabao 4-0 katika muendelezo wa ligi kuu ya NBC, mechi ikipigwa KMC Complex, Dar es Salaam.
Waliotikisa nyavu ni Albert Kangwanda, Ibrahim Bacca, Chadrack Boka na Peter Shalulile.
- Title
- Magoli yote | Yanga SC 4-0 JKT Tanzania | NBC Premier League 24/08/2026
- Runtime
- 6:23
- Date posted
- 6 days ago
- Description
- Yanga SC imeishusia kichapo kizito JKT Tanzania cha mabao 4-0 katika muendelezo wa ligi kuu ya NBC, mechi ikipigwa KMC Complex, Dar es Salaam.
Waliotikisa nyavu ni Albert Kangwanda, Ibrahim Bacca, Chadrack Boka na Peter Shalulile.
- Title
- PRESS SIMBA | Simba SC yathibitisha mechi za nyumbani kuhamia Meja Jenerali Isamuhyo.
- Runtime
- 37:34
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally akizungumza na waandishi wa habari.
Amesema kuanzia sasa mechi zao za nyumbani za Ligi Kuu ya NBC, zitachezwa katika dimba la Meja Jenerali Isamuhyo na mchezo wa kwanza utakuwa dhidi ya wapinzani wao Coastal Union utakaopigwa Agosti 27, 2026.
Aidha, Ahmed amesema kikosi cha Simba SC, kitaondoka nchini Septemba 4, 2026 kuelekea Malawi ili kuwakabili wapinzani wao ambapo mchezo wao dhidi ya Might Wonderers utakuwa ni Septemba 5, 2026.
Azam TV
- Title
- VIWANJANI: Ushindi mwingine kwa Mnyama ugenini! wachambuzi watia neno baada ya matukio ya uwanjani.
- Runtime
- 20:06
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- Wachambuzi wa soka Ramadhani Mbwaduke, Michael Hyera na Khalid Chukuchuku wameeleza kwa undani matukio mawili yaliyoibua mjadala katika mchezo wa NBC Premier League kati ya Singida BS dhidi ya Simba SC.
Tukio la penati na kadi nyekundu aliyooneshwa mchezaji wa Simba SC, Antony Mligo.
Azam TV
- Title
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI | JKT Tanzania yajibu mapigo kwa kocha wa Yanga
- Runtime
- 18:54
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI: JKT Tanzania wajibu mapigo kwa kocha wa Yanga SC, Manqoba Mngqithi ambaye jana Agosti 23, 2026 alionesha ufundi wa kutaja majina ya kila mchezaji kwenye kikosi cha wapinzani wake na kuwachambua pia.
Timu hizo zinakutana leo Agosti 24, 2026 katika dimba la KMC Complex, saa 12:00 jioni LIVE #AzamSports1HD
Ni #Zilizobamba mitandaoni kupitia kipindi cha viwanjani.
#Viwanjani #Zilizobamba
- Title
- Alama tatu Chamazi! Wachambuzi watoa tathmini za kiufundi ushindi wa Azam FC dhidi ya Pamba Jiji.
- Runtime
- 20:24
- Date posted
- 7 days ago
- Description
- Michael Hyera amesema licha ya Pamba Jiji kupoteza mchezo huo, Kocha Francis Baraza alionekana kuridhishwa na kiwango cha kikosi chake, hasa kutokana na namna wachezaji walivyotekeleza majukumu yao uwanjani.
Azam TV

