Mwananchi Digital
Chanzo kifo cha Hashim Kambi afariki baada ya safari ya Tabora, kuzikwa leo Kisutu
- Title
- Chanzo kifo cha Hashim Kambi afariki baada ya safari ya Tabora, kuzikwa leo Kisutu
- Runtime
- 5:54
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- LIVE: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA KUMI NA SABA
- Runtime
- 2:31:31
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- LIVE: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA KUMI NA SABA
- Title
- MMOJA AFA MAJI AKIVUKA KIVUKO CHA MAGOGO, WANANCHI WALALAMIKIA HATARI
- Runtime
- 3:45
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Hai. Mwanaume mmoja ambaye hajafahamika kwa majina wala umri, amefariki dunia kwa kuzama katika Mto Sanya wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro, akidaiwa kuteleza alipokuwa akivuka kivuko cha magogo kinachotumiwa na wananchi kama njia ya muda.
Tukio hilo limetokea leo Aprili 27, 2026 katika mtaa wa Masinonda, kata ya Masama Kusini, likiacha simanzi kwa wakazi wa vijiji vya Mungushi (Hai) na Munge (Siha) vinavyounganishwa na mto huo.
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kilimanjaro, Jeremia Mkomagi, amesema walipokea taarifa ya tukio hilo saa 2:23 asubuhi na kufika eneo la tukio saa 5:38, ambapo walikuta mwili wa marehemu ukielea juu ya maji.
- Title
- CHADEMA YATUMA SALAMU WALIOJITOA UANACHAMA
- Runtime
- 4:25
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Shinyanga. Katika hafla ya kuzindua shughuli za kichama baada la zuio la takribani miezi 10, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Serengeti, kimetuma salamu kwa waliokuwa wanachama ambapo kwa sababu tofauti tofauti wakaamua kujitoa katika chama hicho na kujiunga na vyama vingine.
Akizungumza leo Aprili 26, 2026 katika hafla hiyo na Mwenyekiti wa Chadema kanda maalumu ya Serengeti Lucas Ngoto, iliyofanyika katika Ofisi ya kanda hiyo iliyopo Manispaa ya Shinyanga huku akiwataka wanachama waliopo kushikiria msimamo wao na kutokukubali kuyumbishwa na watu wengine,
“Leo tuko imara kuliko ambavyo tulikuwa jana, kuna baadhi yetu walishuka njiani sisi tukaendelea na safari, walioshuka tuwahurumie sana kwa sababu kushuka kwao hakukutuzuia sisi kuendelea na safari na sasa tumekuja na ngucu mpya” amesema Ngoto.
Pia ameongeza kuwa, “Kuna wwanawake ambao wakiulizwa wanafanya kazi gani wanasema ‘mama wa nyumbani’ hiyo kauli sitaki kuis...
- Title
- #live: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA KUMI NA SABA, APRILI 27, 2026
- Runtime
- 4:12:45
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- Rommy3D afichua ishu ya talaka, ataja kilichowakutanisha na Shilole
- Runtime
- 3:23
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Rommy3D afichua ishu ya talaka, ataja kilichowakutanisha na Shilole
- Title
- PRESHA YA DABI YA KARIAKOO ZANZIBAR YAANZA KUPANDA! ALIYETAKIWA KUJIVUNJA KAKAZA, MDOSE ACHAMBUA ...
- Runtime
- 5:23
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Wadau wa soka wanatarajia kwa hamu kubwa kushuhudia Dabi ya Kariakoo itakayopigwa Aprili 29, 2026, ikiwa ni mara ya pili kwa Yanga na Simba kukutana ndani ya mwaka huu 2026 visiwani Zanzibar. Awali ilikuwa Ligi Kuu Bara iliyomalizika kwa matokeo ya 0-0, lakini safari hii katika fainali ya Kombe la Muungano.
Yanga imefuzu fainali baada ya kuiondoa Azam FC kwa mabao 2-1, huku Simba ikiichapa Mlandege mabao 3-0.
Mchambuzi wa soka, Omary Mdose, ametoa tathmini yake kuelekea pambano hilo la kusisimua.
#samiasuluhuhassan ...
- Title
- ARAFAT, MANGUNGU WAKUTANA KWENYE WARSHA KUPINGA RUSHWA MICHEZONI
- Runtime
- 0:32
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Makamu wa Rais wa Yanga, Arafat Haji na Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, wapo katika warsha iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inayofanyika katika makao makuu ya ofisi hizo Upanga jijini Dar es Salaam.
Warsha hiyo imeandaliwa na TAKUKURU kwa kuwahusisha wadau mbalimbali wa michezo hususani wa mpira wa miguu kwa lengo la kukomesha rushwa michezoni ikiongozwa na mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo, Crispin Chalamila.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsle...
- Title
- RAIS SAMIA MGENI RASMI KONGAMANO LA UVCCM MIAKA 62 YA MUUNGANO
- Runtime
- 2:36:29
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- HECHE: CHADEMA TUMEPITIA MISUKOSUKO, TUTASONGA MBELE TUKIWA IMARA
- Runtime
- 1:46
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Kibamba, Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema licha ya magumu kiliyoyapitia ikiwemo kutofanya shughuli za siasa takribani mwaka mmoja bado kitasimama imara na kusonga mbele.
Juni 10, 2025, Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam ilitoa zuio la Chadema kujihusisha na shughuli za kisiasa kutokana na kesi ya mgawanyo wa mali iliyokuwa ikiendelea.
Hata hivyo, Aprili 15, 2026 ikiwa imepita miezi kumi, Mahakama ya Rufani ilibatilisha uamuzi huo wa Mahakama Kuu na kukiruhusu chama hicho kufanya siasa huku kesi ya msingi ikiendelea.
Leo Jumapili, Aprili 26, 2026, Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara, John Heche ameshiriki mkutano mkuu maalumu uliofanyika jimbo la Kibamba.
Heche amesema chama hicho kitaendelea kujipambanua dhamira yake njema ya kutaka Watanzania waishi maisha bora kutokana na rasilimali zilizopo nchini.
Akitolea mfano, Heche amesema yeye mwenyewe aliwahi kukaa mahabusu kwa karibu...
- Title
- MAFURIKO JANGWANI KUWA HISTORIA, UJENZI WA DARAJA WASHIKA KASI
- Runtime
- 4:01
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema mipango ya Serikali kuboresha miundombinu ya Jiji la Dar es Salaam ina lengo la kuhakikisha barabara zote zinapitika mwaka mzima ili kurahisisha maisha ya wananchi na kukuza uchumi wa taifa.
Ulega amesema hayo leo Jumapili, Aprili 26, 2026 wakati akitoa maelezo hayo mbele ya Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba, aliyekuwa na ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya barabara jijini Dar es Salaam jana.
Ulega ametoa mfano wa ujenzi wa Daraja la Jangwani alilosema kukamilika kwake kutaondoa adha ya kukatika kwa njia ya kutoka Magomeni kuelekea katikati ya jiji na kurejea kwa kusema jambo hilo sasa litakuwa historia.
- Title
- TAZAMA 'VIBE' LA WANACHADEMA WAKIMPOKEA HECHE KIBAMBA
- Runtime
- 2:04
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche, amewasili Kibamba, Dar es Salaam kwa ajili ya mkutano wa chama hicho leo Aprili 26, 2026.
Katika mkutano huo wa kwanza tangu Chadema iondolewe kifungo cha kutofanya shughuli za kisiasa na Mahakama ya Rufani Aprili 15, 2026, wanachama wamempokea kiongozi huyo kwa shangwe na hamasa kubwa, tayari kuanza kwa mkutano huo.
- Title
- SAMIA: HAIWEZEKANI MIFUKO YOTE YA VIJANA KUUNGANISHWA IWE WIZARA YA VIJANA
- Runtime
- 3:36
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema haiwezekani mifuko yote ya vijana kuunganishwa na kuwa chini ya Wizara ya Vijana.
Rais Samia amesema hayo leo, Jumapili, Aprili 26, 2026, aliposhiriki kongamano la vijana wa CCM (UVCCM) Unguja, visiwani Zanzibar, lililokwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
- Title
- KIMEUMANA! WANANCHI DHIDI YA RC CHALAMILA MADAI FIDIA BONDE LA MSIMBAZI MBELE YA DK MWIGULU
- Runtime
- 7:51
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Mwananchi mmoja amewasilisha malalamiko yake mbele ya Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba, akidai hajasaini fidia ya mradi wa Bonde la Msimbazi kutokana na kiwango kidogo alichoelezwa kulipwa, ambacho ni Sh4 milioni.
Akijibu malalamiko hayo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema hadi sio chini ya Sh54 bilioni zimetumika kulipa fidia kwa wananchi waliokuwa wanaishi katika Bonde la Msimbazi.
Aidha, Chalamila ameongeza kuwa hakuna mwananchi yeyote aliyekuwa na sifa ya kulipwa fidia ya ardhi katika eneo hilo, akieleza kuwa taratibu za miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia haziruhusu kulipwa fidia ya ardhi katika Bonde la Mto Msimbazi.
Malalamiko hayo yamewasilishwa leo, Jumapili, Aprili 26, 2026, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Msimbazi katika ziara ya Waziri Mkuu, jijini Dar es Salaam.
- Title
- "KUNA DADA PALE TAMISEMI AMEKUWA KAMA MALAIKA" JAMAA AJILIPUA MBELE YA WAZIRI MKUU MADAI YA FIDIA !
- Runtime
- 6:36
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Dar es Salaam. Wakazi wa Bonde la Mto Msimbazi wameibua malalamiko mazito kuhusu fidia wanazolipwa kupisha mradi wa uendelezaji wa bonde hilo, wakidai kutothaminiwa kwa ardhi yao na viwango vidogo vya fedha vinavyotolewa, mbele ya Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba.
Wakizungumza leo Aprili 26, 2026 mbele ya Waziri Mkuu ambaye alikuwa kwenye ziara ya kukagua ujenzi wa madaraja ya Mkwajuni na Kigogo jijini Dar es Salaam, wananchi hao wamesema licha ya kuupokea mradi huo kwa matarajio ya maendeleo, utekelezaji wake umeacha maumivu makubwa kutokana na kile walichodai ni ukosefu wa haki katika mchakato wa fidia.
- Title
- RC CHALAMILA: NILISEMA KULE SIENDI ..., ZAIDI YA SH10 BILIONI KUJENGA OFISI YA MKUU WA MKOA DAR
- Runtime
- 2:09
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema Serikali imeanza mchakato wa ujenzi wa ofisi mpya za Mkuu wa Mkoa katika eneo la Magomeni, lililokuwa chini ya umiliki wa DDC, kwa lengo la kuboresha mazingira ya kazi na huduma kwa wananchi.
Chalamila amesema mradi huo utagharimu Sh10 bilioni na utahusisha ujenzi wa jengo la kisasa litakaloendana na hadhi ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na mahitaji ya kiutawala yanayoongezeka.
Mkuu huyo wa mkoa ameeleza hayo leo Jumapili Aprili 26, 2026 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Shule ya Msingi Msimbazi katika ziara ya Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba jijini Dar es Salaam.
Amesema tayari fedha hizo zimeshaidhinishwa kufuatia maombi ya mkoa huo kuwa na ofisi mpya yenye miundombinu na muonekano unaoendana na hadhi ya jiji hilo linaloongoza kwa shughuli za kiuchumi.
- Title
- YANGA YAPANIA UBINGWA MUUNGANO CUP! YAITUMIA SALAMU SIMBA
- Runtime
- 1:06
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Afisa Mtendaji Mkuu wa Yanga, Andre Mtine amesema hawawezi kuchagua nani wakutane kwenye mchezo wa Fainali ya Muungano kati ya Simba au Mlandege lakini timu ya inalitaka Kombe hilo kwa mara nyingine.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highlights #cafconfiderationcup #riversunited #mashabiki #yangaleo #yanga #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko #entertainment #music #news #magoliyasimba #magoliyay...
- Title
- IBENGE AANIKA KILICHOIPONZA AZAM IKINYOLEWA NA YANGA MUUNGANO CUP
- Runtime
- 1:46
- Date posted
- 30 days ago
- Description
- Kocha Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, ameweka wazi sababu za kikosi chake kupoteza mechi dhidi ya Yanga.
Ibenge amebainisha kuwa makosa ya kupoteza mipira kwenye maeneo hatari kipindi cha kwanza ndiyo yaliyowagharimu.
Licha ya matokeo hayo, kocha huyo amesisitiza kuwa wamejifunza na watayafanyia kazi makosa hayo kwa ajili ya mechi zinazofuata.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #...
- Title
- BACCA AFUNGUKA MAZITO BAADA YA KUIKANDA AZAM NA KUTINGA FAINALI MUUNGANO CUP
- Runtime
- 1:27
- Date posted
- 30 days ago
- Description
- Beki kisiki wa Yanga na timu ya Taifa, Ibrahim Hamad Bacca, ameweka wazi kuwa akili yao sasa ipo kwenye mechi ya fainali ya Kombe la Muungano utakaopigwa Aprili 29, 2026.
Baada ya kuichapa Azam FC kwenye mechi ya nusu fainali, Bacca amesisitiza kuwa hesabu za timu hiyo ni kumaliza kazi kwa ushindi ili kuendelea kutawala soka la Bongo.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highligh...
- Title
- RAIS SAMIA AKIZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU YA SHIRIKA LA UVUVI TANZANIA (TAFICO)
- Runtime
- 1:22:12
- Date posted
- 30 days ago
- Description
- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizindua Meli ya Kwanza ya Uvuvi wa Bahari Kuu ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), leo Aprili 25, 2026, Kigamboni, Dar es Salaam.
- Title
- MBARONI KWA KUVAA KOFIA YENYE BENDERA MBILI
- Runtime
- 2:24
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Israel. Polisi nchini Israel wamemkamata mwanaume myahudi kwa kuvaa kofia ya kidini (kippah) iliyopambwa kwa bendera za Israel na Palestina, katika tukio lisilo la kawaida lililozua mjadala mkubwa kitaifa.
Mwanaume huyo, Alex Sinclair (53), ambaye ni mwandishi na mhadhiri msaidizi katika Chuo Kikuu cha Hebrew, alisema alikamatwa akiwa amekaa kwenye mgahawa katika mji wa Modiin, takribani kilomita 35 kusini mashariki mwa Tel Aviv.
Kwa mujibu wa maelezo yake kupitia Facebook, Sinclair alisema mtu mmoja wa kidini alimfuata akiwa na hasira na kumwambia kuwa kuvaa kippah hiyo ni kinyume cha sheria, alijaribu kuzungumza naye, lakini mtu huyo alikataa kusikiliza na badala yake akawaita polisi.
Dakika chache baadaye, maofisa wa polisi walifika na kumwambia kwamba kippah yake haikubaliki kisheria na kwamba wangeichukua, baadaye walimpeleka kituo cha polisi, wakampekua na kumuweka rumande kwa muda mfupi bila mawasiliano wala maelezo ya kinachoendelea.
...
- Title
- DC NKINDA AAGIZA UCHUNGUZI SOKO LA NAMANGA
- Runtime
- 3:50
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda, ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani humo kufuatilia malalamiko ya wafanyabiashara wa samaki katika soko la Namanga kuhusu uwepo wa ushuru usio rasmi na ukosefu wa uwazi katika ukusanyaji wa mapato.
Akizungumza katika kikao cha kusikiliza na kutatua kero za wafanyabiashara wa soko hilo, Nkinda amesema ni muhimu uchunguzi wa haraka ufanyike ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.
Amesema “Naiagiza Takukuru kufuatilia takwimu hizi haraka iwezekanavyo na kuniletea uhalisia pamoja na ushauri wa namna ya kumaliza mgogoro huu.”
Mfanyabiashara wa samaki katika soko hilo Irene Mugwa, amesema licha ya kuwa na mtaji mdogo wa Sh500,000, analazimika kulipa ushuru wa hadi Sh390,000 kwa mwezi, kwa kikundi kinachoitwa 'Umoja wa wauza samaki Kahama' (Uwasaka), huku wakipewa stakabadhi za mkono.
Mwenyekiti wa Soko la Namanga Juma Jum...
- Title
- WATU 7 WAKAMATWA KWA MAUAJI YA MUNGU
- Runtime
- 4:26
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya Mungu Mamboleo mkazi wa Ihanga Mkanyageni Tarafa ya Rujewa wilayani Mbarali mkoani humo kwa kumtuhumu kuiba Ng’ombe.
Tukio hilo linadaiwa kutokea Aprili 21 majira ya saa 9 usiku, ambapo kundi la watu hao likiongozwa na Samweli Yohana ‘Fagu’ walivamia kambi ya Ng’ombe na kumkamata na kumshambulia Mungu kwa silaha za jadi hadi kufariki.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo, SACP Benjamin Kuzaga ameeleza kuwa kufuatia tukio hilo, Askari wa kuchunguza matukio ya mauaji, walianza msako na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao.
- Title
- RAIS SAMIA: WASAIDIZI WANGU WALINIAMBIA SIYO MELI YA HADHI YANGU
- Runtime
- 0:56
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Rais Samia Suluhu Hassan ameeleza namna alivyogoma awali kwenda kuzindua meli ya uvuvi baada ya kuambiwa na wasaidizi wake kuwa meli hiyo ni ndogo na haina hadhi ya kuzinduliwa na Rais.
“Nataka nikiri, nilipopata mwaliko nikawaambia watu wangu waende wakaione meli. Waliporudi wakaniambia, ‘Mheshimiwa Rais, hii siyo meli ya hadhi yako, ni meli ndogo tu.’ Nikasema mwambieni Waziri afanye mwenyewe kazi hiyo. Lakini nilipokutana na Waziri (Dk Bashiru Ally-Waziri wa Mifugo na Uvuvi) akaniambia, ‘Ndiyo meli ni ndogo, lakini mambo yake ni makubwa, naomba sana uje,’ na leo nimekuja,” amesema Rais Samia.
Rais Samia ameyasema hayo leo Jumamosi, Aprili 25, 2026, katika hafla ya uzinduzi wa meli ya kwanza ya Serikali ya uvuvi wa bahari kuu ya Shirika la Uvuvi Tanzania (Tafico), iliyofanyika Kigamboni jijini Dar es Salaam.
- Title
- ALIYETARAJIA KUJIFUNGUA ‘PACHA’ WATATU AJIFUNGUA WANNE, AOMBA MSAADA
- Runtime
- 5:54
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Moshi. Mama mkazi wa Newland TPC, mkoani Kilimanjaro, Rachael Simba (28), amejifungua watoto wanne waliozaliwa kabla ya muda (njiti) katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC), tukio linalotajwa kuwa nadra kitaalamu.
Rachel alijifungua watoto hao Aprili 22, 2026 kwa njia ya upasuaji. Amesema hakutarajia kupata watoto wanne kwa mpigo, kwani awali alielezwa kuwa alikuwa na ujauzito wa watoto watatu.
Akizungumza na Mwananchi Digital Ijumaa, Aprili 24, 2026, hospitalini hapo, Rachael amesema watoto hao wanaendelea vizuri chini ya uangalizi maalumu katika chumba cha watoto njiti (Nicu), kutokana na kuzaliwa na uzito pungufu.
- Title
- LIVE: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA KUMI NA SITA
- Runtime
- 3:00:14
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- LIVE: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA KUMI NA SITA
- Title
- Mbowe amwombea msamaha Ole Sabaya kwa wana Hai, asema amebadilika
- Runtime
- 3:44
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- Neema Ngoitiama: Why women must think beyond borders to lead
- Runtime
- 3:42
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- At TCC Plc, Quality Manager Neema Ngoitiama is championing service excellence while urging women professionals to think beyond borders. She highlights international exposure as a powerful tool for building confidence, cultural intelligence, and resilience, empowering women to challenge self-limiting beliefs and recognise that their skills are valuable anywhere in the world.
- Title
- MAMA LISHE ALIYEUAWA KIKATILI AKIWA NA MAZIWA YA MWANAE AAGWA, KUZIKWA ...
- Runtime
- 5:01
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Moshi. Safari ya mwisho ya mama lishe Restituta Moshiro (42) inatarajiwa kuhitimishwa leo katika kijiji cha Shimbi Mashami, wilayani Rombo, ambako atapumzishwa katika nyumba yake ya milele.
Restituta, mama wa watoto wawili akiwemo mtoto mchanga wa miezi saba, alifariki dunia baada ya kuuawa kikatili usiku wa kuamkia Aprili 17, 2026 akiwa katika harakati za kutafuta riziki ya familia yake.
Ibada ya kuaga imefanyika katika Jimbo Katoliki la Moshi, Parokia Teule ya Jina Takatifu la Maria Mnazi Mmoja, ikigubikwa na simanzi na vilio kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki waliokusanyika kutoa heshima za mwisho.
Akizungumza baada ya ibada hiyo, kaka wa marehemu, Christian Moshiro, amesema familia imepata pigo kubwa na bado inaumia kutokana na mazingira ya kifo hicho cha kusikitisha.
Baada ya ibada, mwili wa Restituta umesafirishwa kuelekea Rombo kwa mazishi, ukiacha nyuma majonzi makubwa na simulizi ya mama aliyepoteza maisha akiwa bado na ndot...
- Title
- SIRI YA IRAN YAFICHUKA, TRUMP AKIDAI MGAWANYIKO
- Runtime
- 2:52
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Iran. Rais wa Donald Trump amedai kuwa utawala wa Iran umegawanyika sana, akieleza hivyo alipoongeza muda wa kusitisha mapigano, ili kutoa nafasi kwa Tehran kuwasilisha pendekezo la pamoja, hata hivyo wachambuzi wengi wanaona hali hiyo si rahisi kama anavyoeleza, wakisema uongozi wa Iran unaonekana kuwa na mshikamano zaidi kuliko, inavyodaiwa.
Kauli ya Trump ilikuja baada ya Iran, kutohudhuria duru ya pili ya mazungumzo nchini Pakistan na Makamu wa Rais wa Marekani, jambo ambalo Ikulu ya White House ililitafsiri kama ishara ya mgawanyiko ndani ya uongozi wa Iran, huku Tehran imesisitiza haitarejea mezani kwa mazungumzo hadi Marekani itakapositisha vikwazo dhidi, ya bandari zake.
Wataalamu wa siasa za Mashariki ya Kati wanapinga tafsiri hiyo, wakisema licha ya shinikizo la vita na vifo vya baadhi ya viongozi wakuu, mfumo wa uongozi wa Iran bado unaonyesha umoja katika maamuzi ya kimkakati na mazungumzo, ya kidiplomasia.
Baada ya kuuawa kwa Kiongozi...
- Title
- SAMIA: NITAUBEBA MZIGO HUU KWA UJASIRI, KUJIAMINI NA TAHADHARI KUBWA YALIYOTOKEA OKTOBA 29
- Runtime
- 1:27
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Rais Samia Suluhu Hassan, amesema hakutarajia kutokea kwa kadhia hiyo nchini katika kipindi chake cha uongozi, akieleza kuwa hali hiyo imembebesha mzigo mkubwa wa uwajibikaji.
Akizungumza wakati akipokea ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani, leo Aprili 23, 2026, Rais Samia amesema, ataubeba mzigo huo kwa ujasiri na tahadhari kubwa.
“Nataka nikiri kwamba, mimi binafsi sikutarajia kadhia hii ingetokea kwenye nchi yetu kipindi hiki nikiwa kiongozi mkuu wa nchi, jambo hili limenitwisha mzigo mzito mabegani kwangu,” amesema.
- Title
- TUME YA KUCHUNGUZA MATUKIO: HAKUNA UTHIBITISHO WA UWEPO WA MAKABURI YA HALAIKI
- Runtime
- 2:01
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, Jaji Othman Chande amesema uchunguzi uliofanyika umebaini hakuna uthibitisho wa uwepo wa makaburi ya halaiki kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari vya kimataifa.
Akiwasilisha matokeo ya uchunguzi, Jaji Chande amesema uchunguzi wa kina umebaini madai hayo hayana ukweli.
Amesema tume ilitembelea na kukagua eneo la Makaburi ya Kondo, kufanya mahojiano na wasimamizi pamoja na kushirikisha wataalamu mbalimbali kufanya uchunguzi wa kisayansi, ikiwemo matumizi ya picha za satelaiti.
Amesema pamoja na hatua hizo, mazingira ya eneo hilo likiwa limezungukwa na makazi ya watu na kulindwa muda wote yalisaidia kufikia hitimisho kuwa hakuna ushahidi wa kuwepo makaburi ya halaiki.
“Hivyo kwa kuzingatia hali halisi ilivyo pamoja na taarifa za uchunguzi wa kisayansi, tume ilibaini madai hayo hayakuweza kuthibitika,” amesema.
- Title
- TUME: WATU 518 WALIFARIKI GHASIA ZA OKTOBA 29, MAJERUHI ...
- Runtime
- 13:30
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imesema kuwa vifo vilivyotokana na ghasia hizo ni 518 ambao wanaume 490 sawa na asilimia 94.6, wanawake 28 sawa na asilimia 5.4, ambapo katika vifo hivyo watoto walikuwa 21.
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu, Mohamed Chande leo Alhamisi, Aprili 23, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akiwasilisha akipokea Ripoti ya Tume hiyo kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan..
“Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa na vifo vingi zaidi ikiwa na vifo 182 ikiuatiwa na Mwanza 90, Mbeya 80 na Arusha 53,” amesema Jaji Chande.
- Title
- RAIS SAMIA AKIPOKEA RIPOTI YA TUME YA KUCHUNGUZA MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI - UCHAGUZI MKUU - 2025
- Runtime
- 2:51:07
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- RAIS SAMIA AKIPOKEA RIPOTI YA TUME YA KUCHUNGUZA MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI - UCHAGUZI MKUU - 2025
- Title
- TUME: KILICHOTOKEA OKTOBA 29 SIYO MAANDAMANO YA AMANI, NI GHASIA
- Runtime
- 13:31
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Jaji mstaafu Mohammed Chande, amesema tume imebaini kuwa kilichotokea kabla na baada ya uchaguzi ni ghasia, siyo maandamano ya amani kama inavyodaiwa nje.
“Tume imepata ushahidi usio na shaka kwamba matukio ya ghasia za Oktoba 29 yalipangwa, yaliratibiwa, yalifadhiliwa na kutekelezwa na watu waliopata mafunzo, waratibu walitumia mbinu mbalimbali, ikiwemo kuwatumia watu wasio na ufahamu wa kina na vijana waliokata tamaa,” amesema.
Jaji Chande amebainisha hayo leo, Alhamisi, Aprili 23, 2026, Ikulu, jijini Dar es Salaam, alipozungumza kabla ya kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
- Title
- UTEKAJI, KUJITEKA, MADAI YA KATIBA MPYA, GHARAMA ZA MAISHA ZATAJWA CHANZO CHA VURUGU OKTOBA 29
- Runtime
- 7:34
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza matukio ya Oktoba 29, 2025 Jaji Mohamed Chande amesema maandamano ya vurugu zilizotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 wahusika walikuwa na malengo makuu matatu.
Akiwasilisha ripoti ya Tume hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi, Aprili 23, 2026 Jaji Chande amesema lengo la kwanza lilikuwa kuzuia uchaguzi usifanye na ndio sababu makundi ya waandamanaji walivamia kwenye vituo vya kupigia kura.
Amesema makundi hayo yalivamia na kuharibu vifaa vya kupigia kura, kushambulia askari polisi waliokuwa wakilinda kwenye maeneo hayo.
Kwa mujibu wa Jaji Chande lengo lingine lilikuwa ni kufikisha ujumbe kwa Serikali kutokana na changamoto ya gharama za maisha, uwepo wa demokrasia na haki sawa kwa vyama vya siasa pamoja na madai ya Katiba mpya.
Amesema kwa muda mrefu kumekuwepo kilio cha madai ya Katiba mpya hivyo, vurugu hizo zililenga kufikisha kilio...
- Title
- JAJI CHANDE: BAADHI YA PICHA NA VIDEO HAZIKUWA HALISI
- Runtime
- 2:42
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Wakati jamii ikiendelea kuwa na maswali mengi kuhusu video ambazo zimekuwa zikisambaa mitandaoni kuhusu kilichotokea katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025, Tume ya Rais ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani katika uchaguzi huo, imesema kulikuwa na picha za kweli na za upotoshaji.
Akiwasilisha ripoti ya tume hiyo kwa Rais Samia Suluhu Hassan, wenyekiti wa Tume hiyo Jaji mstaafu Mohamed Chande, amesema baadhi ya picha na video hizo zilikuwa za kweli na zingine zilikuwa zimetengenezwa.
“Uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya picha zilizosambaa zilikuwa za kweli na zingine hazikuwa za kweli,” amesema Jaji Chande.
Katika maelezo yake, Jaji Chande amesema baadhi ya video zilizosambazwa zaidi katika mitandao ya kijamii ni zile zilizotengenezwa akitolea mfano picha iliyosambazwa zaidi ikionesha miili ya watu kwenye mifuko ya bluu.
- Title
- TUME YATAJA MAENEO YALIYOATHIRIKA ZAIDI GHASIA ZA OKTOBA 29
- Runtime
- 4:37
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imebainisha kuwa ilifanya uchunguzi katika maeneo 202 yaliyoathirika zaidi, yakihusisha wilaya 21 kutoka mikoa 11 ya Tanzania Bara.
Akizungumza leo Alhamisi Aprili 23, 2026, Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi ripoti kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Mohammed Chande amesema uchunguzi huo ulilenga kubaini chanzo cha matukio ya ghasia pamoja na kutoa mapendekezo ya namna ya kuimarisha amani nchini.
Ametaja maeneo yaliyoathirika zaidi ikiwemo Dar es Salaam, Mbeya, Songwe, Mwanza, Geita, Arusha, Iringa, Dodoma, Shinyanga, Ruvuma na Kimara.
“Uchunguzi ulihusisha maeneo 202 yaliyoathirika zaidi katika wilaya 21 na mikoa 11. Lengo lilikuwa kupata taswira halisi ya matukio na sababu zilizochangia uvunjifu wa amani,” amesema Jaji Chande.
Aidha, amesema tume hiyo ilitembelea pia Zanzibar na mkoa...
- Title
- HOW TANZANIA’S GOVERNMENT-OWNED TELECOM COMPANY MADE A TURNAROUND FROM BILLIONS IN LOSSES
- Runtime
- 44:55
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- In this exclusive interview, Moremi Marwa, the Director General of the Tanzania Telecommunications Corporation Limited (TTCL), discusses his mandate to turn around the state-owned strategic telecommunications entity, the challenges of operating within a competitive market, and his vision for TTCL's role in Tanzania's digital economy.
- Title
- MBUNGE MUSUKUMA: TUMUOMBE TRUMP AREGEZE BEI YA MAFUTA ISHUKE, TUSIINGIE KWENYE MTEGO HUU ...
- Runtime
- 4:40
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- #live: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA 15, APRILI 23, 2026
- Runtime
- 1:38:30
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- RAIS SAMIA AKIPOKEA RIPOTI YA TUME YA KUCHUNGUZA MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI - UCHAGUZI MKUU - 2025
- Runtime
- 12:53
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- RAIS SAMIA AKIPOKEA RIPOTI YA TUME YA KUCHUNGUZA MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI - UCHAGUZI MKUU - 2025
- Title
- HIKI HAPA KILICHOMREJESHA SALUM MAYANGA KUWA KOCHA MKUU WA MBEYA CITY
- Runtime
- 2:14
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Afisa Habari wa Mbeya City, Gwamaka Mwankota amefafanua sababu za kumvuta Salum Mayanga kuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo baada ya kuachana na mtangulizi wake, Mecky Maxime.
Mayanga alitua kikosini humo akikumbukwa kuinoa timu hiyo mapema msimu uliopita ikiwa Championship kabla ya kutimkia Mashujaa FC na nafasi yake kuzibwa na Malale Hamsin aliyepanda nayo daraja kisha kutemwa mapema msimu huu.
Akizungumza Aprili 22, 2026, Mwankota amesema Mayanga ndiye alihusika kwa asilimia kubwa kuipandisha timu na hata alipoomba kuondoka walimpa baraka zote na sasa amerejeshwa tena.
- Title
- KWA NINI TTCL HAIACHANI NA BIASHARA YA SIMU LICHA YA UTAWALA KIDUCHU SOKONI?
- Runtime
- 36:27
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mahojiano maalumu na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Moremi Marwa.
- Title
- #live: MJADALA BUNGENI KUHUSU BAJETI YA WIZARA YA NISHATI
- Runtime
- 44:43
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- #live: MJADALA BUNGENI KUHUSU BAJETI YA WIZARA YA NISHATI
- Runtime
- 1:28:46
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- VITA YA MAREKANI, IRAN YAINGIA HATUA MPYA...
- Runtime
- 2:11
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Washington. Rais wa Marekani Donald Trump ameongeza muda wa makubaliano ya kusitisha mapigano na Iran, hatua iliyokuja baada ya siku yenye msukosuko wa diplomasia mjini Washington, huku juhudi za kumaliza vita zikiendelea kuwa, na sintofahamu.
Siku ya Jumanne ilianza kwa matarajio makubwa, ambapo ndege ya Air Force Two ikiwa tayari kumpeleka Makamu wa Rais JD Vance, kwenda Islamabad kwa mazungumzo ya amani kati ya Marekani na Iran, hata hivyo safari hiyo haikufanyika na mazungumzo, yakaahirishwa.
Baadaye, Trump alitangaza kuongeza muda wa kusitisha mapigano uliokuwa unatarajiwa kuisha Jumatano jioni, akisema Iran imepewa nafasi zaidi ya kuwasilisha mapendekezo ya pamoja ya kumaliza, vita hiyo.
Katika siku hiyo, Ikulu ya Marekani ilikumbwa na sintofahamu baada ya Iran kutotoa uthibitisho wa kushiriki mazungumzo, hali iliyoiweka Washington katika wakati mgumu wa kuamua iwapo imtume Vance bila uhakika wa ushiriki, wa Tehran.
Dalili za ku...
- Title
- ASKARI JELA SIKU 30, KASHFA YA KUDHALILISHA ALAMA YA KIDINI
- Runtime
- 1:55
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Lebanon. Wanajeshi wa Israel wamechukuliwa hatua za kinidhamu baada ya tukio la kuharibu sanamu ya Yesu kusini mwa Lebanon, tukio lililosababisha hasira kubwa mtandaoni baada ya picha kusambaa kwa kasi.
Jeshi la Israel Defense Forces (IDF) limesema askari aliyepiga sanamu ya Yesu kwa nyundo na mwenzake aliyepiga picha ya tukio hilo watatumikia kifungo cha kijeshi cha siku 30.
Aidha, wanajeshi hao wawili wameondolewa katika majukumu ya mapambano, kufuatia uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo, huku hatua zaidi zikitarajiwa dhidi yao.
IDF pia imesema, wanajeshi wengine sita waliokuwepo eneo la tukio lakini wakashindwa kuzuia au kuripoti tukio hilo, watashughulikiwa kwa njia tofauti.
Tukio hilo lilitokea katika kijiji cha Debel kusini mwa Lebanon na kulaaniwa vikali, huku Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akieleza kushtushwa na kusikitishwa na kilichotokea.
Katika taarifa yake, IDF ilisema kitendo hicho kilikiuka kabisa ...
- Title
- #live: BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA KUMI NA NNE, APRILI 22, 2026
- Runtime
- 3:51:03
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
- Title
- LIVE:RAIS SAMIA AKIFUNGUA KONGAMANO LA KITAIFA LA MAMALISHE NA BABALISHE DAR.
- Runtime
- 2:02:37
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- RAIS SAMIA AKIFUNGUA KONGAMANO LA KITAIFA LA MAMALISHE NA BABALISHE, TAREHE 21/04/2026, DAR.

