Azam TV
Al Hilal 2-0 Tusker FC | Highlights | CECAFA Kagame Cup 2026 - 26/07/2026
- Title
- Al Hilal 2-0 Tusker FC | Highlights | CECAFA Kagame Cup 2026 - 26/07/2026
- Runtime
- 9:45
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #KagameCup2026: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa CECAFA Kagame Cup 2026 kati ya Al Hilal dhidi ya Tusker ya Kenya.
Wafungaji ni Kamaradini Mamudu na Salim Adams
FT: Al Hilal SC 2-0 Tusker FC
Saa 1:00 usiku ni Rayon Sports dhidi ya KVZ SC, LIVE #AzamSports1HD
#CECAFAKagameCup #CECAFAKagameCup2026 #KombeLakagame #AlHilal #Tusker
- Title
- Highlights | Manyara 52 - 30 Arusha (Wanawake) | Basketball Taifa Cup 26/07/2026
- Runtime
- 14:34
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Timu ya Mkoa wa Manyara Wanawake imepata ushindi wa pointi 52 dhidi ya Arusha katika muendelezo wa michuano ya Kikapu, Taifa Cup inayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.
Azam TV
- Title
- Sakata la usajili wa Girumugisha, Kocha Al Hilal atoa neno
- Runtime
- 2:17
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- KUTOKA RWANDA: Kufuatia tetesi za usajili zinazomuhusu kiungo wa Al Hilal SC ya Sudan, Jean Claude Girumugisha, kocha wa klabu hiyo Guy Bukasa amefunguka mustakabali wa mchezaji huyo na kile timu yao inatamani kitokee kwenye biashara hiyo.
Kwa sasa Al Hilal ipo uwanjani ikimenyana na Tusker kwenye mchezo wa #CECAFAKagameCup2026.
#CECAFA2026 #CECAFAKagameCup2026
- Title
- MSHIKEMSHIKE 23/07/2026 - AZAM TV
- Runtime
- 49:47
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Clifford Ndimbo afunguka mustakabali wa VAR nchini
- Runtime
- 40:52
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- SPORTS AM: Ofisa Habari wa TFF, Clifford Mario Ndimbo amezungumzia mwenendo wa mafunzo ya VAR ambayo yanahusisha waamuzi 18 huku akitaja utofauti kati ya VAR na VS ambayo ilitajwa na Rais wa Shirikisho hilo, Wallace Karia.
#SportsAM #Ndimbo #TFF
- Title
- NBC DODOMA MARATHON 2026 | Tanzania yatawala kilometa 10
- Runtime
- 2:12
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #NBCDodomaMarathon2026 | Kwenye mbio za umbali wa Kilometa 10, nafasi ya kwanza kwa wanawake ilienda kwa Neema Mswati, nafasi ya pili imebebwa na Anna Dolomongo huku nafasi ya pili ikenda kwa Jackline Posiani.
Kwa wanaume, nafasi ya kwanza imeenda kwa Jumanne Mnada, nafasi ya pili imekwenda kwa Augustino Daniel na nafasi ya tatu imekwenda kwa John Wele.
#NBCDodomaMarathon2026 #KataWese
- Title
- NBC DODOMA MARATHON 2026 | Tanzania yang'ara Kilometa 21
- Runtime
- 1:33
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #NBCDodomaMarathon2026 | Kwenye Kilometa 21, Magdalena Shauri kutoka Tanzania ndiye ameibuka kinara kwa upande wa Wanawake huku nafasi ya pili ikishikwa na Dorin Kibeti kutoka Kenya na nafasi ya tatu ikibebwa na Luduina Cheptichi pia kutoka Kenya.
Kwa upande wa wanaume, nafasi ya kwanza imeshikwa na Bernard Geay kutoka Tanzania, nafasi ya pili imekwenda kwa Simon Kelenzoyoke kutoka Kenya huku nafasi ya tatu ikibebwa na Michael Geay kutoka Tanzania.
#NBCDodomaMarathon2026 #KataWese
- Title
- NBC DODOMA MARATHON 2026 | Wakenya wabeba medali zote mbio Kilometa 42
- Runtime
- 2:06
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #NBCDodomaMarathon2026 | Wakenya wauwasha moto kwenye NBC Dodoma Marathon kwa kunyakua medali za mshindi wa kwanza, mshindi wa pili na mshindi wa tatu katika mbio za Kilometa 42.
Agness Ngolo ndiye mshindi wa kwanza, Josinta Chepkoech ameshika nafasi ya pili huku Joyce Kemuma akishika nafasi ya tatu huku wote wakitokea Kenya ikiwa ni kwa upande wa wanawake.
Kwa wanaume nafasi ya kwanza imekwenda kwa Edwin Kibetikoech, nafasi ya pili imekwenda kwa Vitalis Kibioti huku nafasi ya tatu ikienda kwa James Kariuki.
#NBCDodomaMarathon2026 #KataWese
- Title
- NBC DODOMA MARATHON 2026 | Waziri Mkuu Mwigulu azitaja Simba, Yanga kwenye marathon
- Runtime
- 3:21
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #NBCDodomaMarathon2026 | “What a Marathon!”
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema NBC Dodoma Marathon imeendelea kuwa zaidi ya tukio la michezo, kwani imekuwa jukwaa muhimu linalochochea maendeleo ya uchumi, kuhamasisha afya bora na kuunganisha jamii.
Akizungumza katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, Dkt. Nchemba amesisitiza kuwa Marathon hiyo imejijengea nafasi kubwa kama kichocheo cha shughuli za kiuchumi huku akiendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika mazoezi na kuishi maisha yenye afya.
- Title
- Raundi mbili za maajabu | Dullah Mbabe vs Hussein Itaba | VITASA Dar Boxing Derby
- Runtime
- 10:00
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- DAR BOXING DERBY: Unajua kilichotokea kwenye pambano kati ya Dullah Mbabe na Hussein Itaba?
Hizi ni raundi mbili zilizokuwa na moto wa aina yake kati ya kumi zilizopigwa, kila mmoja akilamba sakafu kwa wakati wake….
Mwishoni wakati wa matokeo kuna mmoja ameshangilia sare… umemuona?
Full fight tumekuwekea Youtube.
Ilikuwa ni Dar Boxing Derby uhondo wote ukitokea hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama #DullahMbabe #HusseinItaba
- Title
- VITASA | Juma Choki alivyompiga Tony Rashid na kuchukua Crown Mtoa Roho | Dar Boxing Derby 24/7/2026
- Runtime
- 36:43
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- TONY RASHID vs JUMA CHOKI | Bondia Juma Choki ameshinda gari aina ya Crown (Crown Mtoa Roho) baada ya kumshinda kwa pointi Tony Rashid , katika Usiku wa Vitasa Dar Boxing Derby.
Hili ndilo lilikuwa pambano kuu usiku huu...
Tukio limefanyika Julai 24 ndani ya ukumbi wa EACLC , ubungo Dar es Salaam.
Tazama ilivyokuwa...
- Title
- Tazama kilichotokea pambano la Dullah Mbabe vs Hussein Itaba | VITASA | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 40:13
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Ni sare, kati ya Dullah Mbabe na Hussein Itaba, pambano zito la raundi 10, kila mmoja akilamba sakafu kwa wakati wake.
Ilikuwa ni Dar Boxing Derby uhondo wote ukitokea hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama @semunyu_peaktimemedia
- Title
- Simba SC 0-0 Mogadishu City Club | Highlights | CECAFA Kagame Cup 24/07/2026
- Runtime
- 7:54
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Simba SC imekabwa koo na kulazimishwa suluhu na Mogadishu City Club ya Somalia, katika mchezo wake wa kwanza wa Kombe la Kagame 2026, ukipigwa kwenye Dimba la Kigali, Rwanga.
Kwenye mchezo huu Simba imewatumia baadhi ay nyota wake wapya akiwemo Ibrahim Doumbia , Cooper, Kelvin Nashon na wengine.
Tazama highlights.
- Title
- VITASA | Issa Mollel vs Adam Peter | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 26:48
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Adam Peter amemkaanga Issa Mollel kwa pointi, katika pambano la raundi nane ambalo lilikuwa ni la moto zaidi kwa Mollel.
Ilikuwa ni Dar Boxing Derby uhondo wote ukitokea hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama @semunyu_peaktimemedia
- Title
- VITASA | Mohamed Chappo vs Bakari Kibiki | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 22:25
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Tazama raundi zote sita za Mohamed Chappo kumpiga Bakari Kibiki kwa pointi...
Ilikuwa ni Dar Boxing Derby uhondo wote ukitokea hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama @semunyu_peaktimemedia
- Title
- Singida BS 0-2 Jamusi | Highlights | CECAFA Kagame Cup 25/07/2026
- Runtime
- 9:14
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mabingwa watetezi, Singida BS wamepigwa chuma mbili bila majibu na Jamusi United kutoka Sudan Kusini, mchezo wa Kundi B, michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea nchini Rwanda.
Magoli yamefungwa na Laurent Ramzani na Mario Tabani.
- Title
- Magoli | Singida BS 0-2 Jamusi | CECAFA Kagame Cup 25/07/2026
- Runtime
- 2:57
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mabingwa watetezi, Singida BS wamepigwa chuma mbili bila majibu na Jamusi United kutoka Sudan Kusini, mchezo wa Kundi B, michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea nchini Rwanda.
Magoli yamefungwa na Laurent Ramzani na Mario Tabani.
- Title
- VITASA | Debora Mwenda vs Dorothea Muhoza | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 20:43
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- VITASA | Sarah Alex vs Dorosia Mazige | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 18:55
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Sarah Alex amepata ushindi wa pointi dhidi ya Dorosia Mazige lakini cha moto amekiona. Tazama raundi nane za nguvu..
Hii ni Dar Boxing Derby ikifanyika hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama @semunyu_peaktimemedia
- Title
- VITASA | Hamza Mengo vs Juma Tondola | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 21:02
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Tazama raundi zote sita, Juma Tondola akimuadhibu Hamza Mengi kwa pointi.
Hii ni Dar Boxing Derby ikifanyika hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama @semunyu_peaktimemedia
- Title
- VITASA | Mrisho Mzezele vs Iddi Hamisi | Dar Boxing Derby 24/07/2026
- Runtime
- 19:42
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Idd hamis amempiga Mrisho Mzezele kwa pointi
Hii ni Dar Boxing Derby ikifanyika hapa East Africa Commercial & Logistics Center, Ubungo Dar es Salaam na kukufikia LIVE #AzamSports3HD.
#DarBoxingDerby #VitasaNight #Vitasa #UsikuWaVitasa #CrownMtoaRoho #SitakiLawama @semunyu_peaktimemedia
- Title
- APR FC 0-5 Gor Mahia FC | Highlights | CECAFA Kagame Cup 24/07/2026
- Runtime
- 12:24
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #KagameCup2026 Magoli yote matano waliyoadhibiwa APR: Wafungaji ni Mike Kibwage, Patrick Essombe, Paul Okoth, Lesley Owino, Ebenezer Assifuah.
FT: APR FC 0-5 Gor Mahia
#CECAFAKagameCup #CECAFAKagameCup2026 #KombeLakagame #APRFC #GorMahia #APRGorMahia
- Title
- Yanga SC yatambulisha mashine tatu kutoka nje ya Tanzania; Hersi awasainisha mikataba hadharani
- Runtime
- 9:58
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Rais wa Yanga SC, Hersi Said ametambulisha wachezaji wapya watatu kutoka nje ya Tanzania, katika tukio lililokuwa LIVE #azamTV
Wachezaji hao ni Cheikh Ibrahim Toure, Albert Kangwanda na Housseine Zakouani.
Huyu hapa Hersi akieleza sifa za wachezaji hao...
- Title
- Magoli | APR FC 0-5 Gor Mahia FC | CECAFA Kagame Cup 24/07/2026
- Runtime
- 6:41
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #KagameCup2026 Magoli yote matano waliyoadhibiwa APR: Wafungaji ni Mike Kibwage, Patrick Essombe, Paul Okoth, Lesley Owino, Ebenezer Assifuah.
FT: APR FC 0-5 Gor Mahia
#CECAFAKagameCup #CECAFAKagameCup2026 #KombeLakagame #APRFC #GorMahia #APRGorMahia
- Title
- Vipers 3-0 Garde Republicaine | CECAFA Kagame Cup 24/07/2026
- Runtime
- 8:16
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Faruku Miya amepiga chuma mbili, Vipers ikianza kwa kicheko michuano ya Kombe la Kagame 2026 inayofanyika Kigali nchini Rwanda.
Goli la tatu limefungwa na Abdul Watambala..
Tazama highlights...
- Title
- Magoli | Vipers 3-0 Garde Republicaine | CECAFA Kagame Cup 24/07/2026
- Runtime
- 3:40
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Faruku Miya amepiga chuma mbili, Vipers ikianza kwa kicheko michuano ya Kombe la Kagame 2026 inayofanyika Kigali nchini Rwanda.
Goli la tatu limefungwa na Abdul Watambala..
- Title
- CECAFA KAGAME CUP | Medie Kagere achambua makundi yote, ataja kundi la kifo
- Runtime
- 8:00
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- KAGAME CUP 2026 | Medie Kagere anachambua makundi yote manne, huku akilitaja kundi C kama kundi la kifo.
Je, wewe ni kundi gani hapa unaliona gumu zaidi?
Matangazo haya unayapata kwa lugha tatu tofauti. Ambazo ni Kiswahili, Kiingereza na Kinyarwanda.
#CECAFAKagameCup #CECAFAKagameCup2026
- Title
- Highlights | Iringa 49-84 Pwani (Wanaume) | Basketball Taifa Cup 24/07/2026
- Runtime
- 11:04
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Timu ya Mkoa wa Pwani Wanaume imepata ushindi wa pointi 84-49 dhidi ya Iringa katika muendelezo wa michuano ya Kikapu, Taifa Cup inayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.
Azam TV
- Title
- VIWANJANI: Klabu zaongeza kasi ya usajili kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu NBC 2026/2027.
- Runtime
- 1:15:36
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Mchambuzi wa soka Abissay Stephen amesema usajili umechangamka na unaenda kwa kasi kwa sababu muda umeenda.
Amesema timu zimeongeza kasi ya kufanya usajili ili kukidhi mahitaji yao ndani ya dirisha hili la usajili zikilenga kuimarisha vikosi kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC.
#NBCPL #Viwanjani
- Title
- VITASA | CDF CUP2026 | 21/07/2026 | Maximilian Oloo vs Haruna Swanga.
- Runtime
- 22:28
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Ni raundi tatu za nguvu kati ya Maximilian Oloo na Haruna Swanga, ambaye ameshinda kwa pointi.
Ni mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi upande wa ngumi, yaliyofanyika viwanja vya Twalipo
- Title
- CECAFA kutumika kama kipimo cha maandalizi ya msimu mpya 2026/2027
- Runtime
- 1:02:29
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- VIWANJANI: "yenyewe ni mashindano, lakini ni sehemu ya pre season"
Ni maoni ya mchambuzi wa soka @ramadhani_mbwaduke akieleza kuwa mashindano hayo yanatoa nafasi kwa timu kujenga kikosi, kujaribu mifumo ya uchezaji na kuongeza utayari wa timu kabla ya msimu kuanza rasmi.
Azam TV
- Title
- Waziri Masauni akagua ujenzi wa uwanja mpya Chalinze, atoa maagizo
- Runtime
- 2:35
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Hamad Masauni ameagiza ujenzi wa uwanja wa mpira ulioko Chalinze mkoani Pwani ukamilishwe kwa wakati ili kuharakisha maendeleo ya michezo mkoani humo.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete amezikaribisha timu kufanya mazoezi kwenye uwanja mara utakapokamilika.
Ujenzi wa uwanja huo utakaobeba watazamaji 20,000 umefikia asilimia 45 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu.
- Title
- VITASA | CDF CUP 2026 | Abdallah Mfaume vs Mohamed Juma | 21/07/2026
- Runtime
- 12:32
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Ni raundi tatu za nguvu kati ya Abdallah Mfaume na Mohamed Juma, ambaye ameshinda kwa pointi.
Ni mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi upande wa ngumi, yakifanyika viwanja vya Twalipo
- Title
- Highlights | Arusha 65-46 Tanga (Wanawake) | Basketball Taifa Cup 22/07/2026
- Runtime
- 13:49
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Timu ya Mkoa wa Arusha Wanawake imepata ushindi wa pointi 65-46 dhidi ya Tanga katika muendelezo wa michuano ya Kikapu, Taifa Cup inayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.
Tazama mambo yalivyokuwa
- Title
- Highlights | Nyika 0-2 Jeshi la Akiba | CDF CUP 2026
- Runtime
- 7:15
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- VITASA | CDF CUP 2026 | Steven Anastazia vs Mwalami Salum | 21/07/2026
- Runtime
- 9:05
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- VITASA | CDF CUP 2026 | Hassan Mrutu vs Hamad Issa | 21/07/2026
- Runtime
- 11:40
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Ally Kamwe: Tunakuja kama kifo
- Runtime
- 1:53
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- YANGA SC : “…tunakuja kama kifo”
Ally Kamwe anasema leo Julai 22 ndiyo ilikuwa mwisho wa kutangaza “bunduki za nyumbani”, na kuanzia kesho Julai 23 ndiyo wataanza kufungua boksi la silaha hatari kutoka nje ya Tanzania.
Huyu hapa Ally Kamwe akitema cheche kuhusu usajili ndani ya klabu ya Yanga...
- Title
- MSHIKEMSHIKE 22/07/2026 - AZAM TV
- Runtime
- 49:34
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Tuzo na makombe kwa waliong'ara CDF Cup 2026
- Runtime
- 1:27:13
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- VITASA | CDF CUP 2026 | Credo Peter vs Sikudhani Simon | 21/07/2026
- Runtime
- 11:42
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Shuhudia jinsi Credo Peter wa Kamandi ya Jeshi la Kujenga Taifa (MMJKT) ameshinda kwa pointi dhidi ya Sikudhani Simon kutoka Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi.
Ngumi zilikuwa LIVE #AzamSports2HD
#CDFCup2026 #CDFCup #MashindanoYaMkuuWaMajeshi #JeshiLaAkiba #Vitasa #Ngumi #Boxing #CredoSikudhan
- Title
- Magoli | JKT 3-1 Ngoma | Fainali | CDF Cup 22/07/2026
- Runtime
- 3:59
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- #CDFCUP2026 Haya hapa magoli yaliyowapa ubingwa Kamandi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) dhidi ya Kamandi ya Jeshi Makao Makuu (Ngome/DFHQ).
Sema neno kuhusu golikipa wa Ngome...
FT: JKT 3-1 Ngome
Basketball Taifa Cup inaendelea #AzamSports3HD
#CDFCup2026 #CDFCup #MashindanoYaMkuuWaMajeshi #JeshiLaAkiba #JKT #MMJKT #Ngome #DFHQ #JKTNgome
- Title
- VITASA | CDF CUP 2026 | Mwanandeje vs Said Kanenda | TKO | 21/07/2026
- Runtime
- 9:30
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- TKO ya Said Kanenda dhidi ya Mwanandeje. Hii ni CDF Cup, mapambano yakipigwa tika viwanja vya Twalipo, Temeke Dar es Salaam.
Ngumi hizi zilikuwa LIVE #AzamSports2HD
#CDFCup2026 #CDFCup #MashindanoYaMkuuWaMajeshi #JeshiLaAkiba #Vitasa #Ngumi #Boxing #CredoSikudhan
- Title
- Hotuba kamili ya Waziri Makonda akizindua rasmi Basketball Taifa Cup 21/07/2026
- Runtime
- 12:48
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda akitoa neno katika ufunguzi rasmi wa michuano ya kikapu ya Taifa Cup inayofanyika Chinangali Park Dodoma.
Katika hotuba yake makonda ametoa pongezi kwa Azam Media kwa udhamini wao kwenye michuano hii pamoja na kuwataka viongozi wa mikoa ambayo haijapeleka timu, kujitathmini kama wanatosha kwenye nafasi zao.
- Title
- Waziri Makonda awapa 'makavu live' viongozi hawa wa kikapu | Taifa Cup 21/07/2026
- Runtime
- 2:59
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- TAIFA CUP 2026 | “…ndio mwisho wa uongozi wenu”
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda akitoa maelekezo kwa viongozi wa mikoa ambayo haijapeleka timu kwenye mashindano ya Taifa Cup yanayoendelea Dodoma, akisema “..mjihesabu uongozi wenu umekufa”.
Maelekezo haya yanahusu pia viongozi ambao mikoa yao haina mashindano.
#TaifaCup2026 #Basketball #Kikapu #BasketballTaifaCup #TBF #DodomaMwanza
- Title
- Hotuba ya Hasheem Thabeet katika ufunguzi rasmi wa basketball Taifa Cup 21/07/2026
- Runtime
- 3:17
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- TAIFA CUP 2026 | Neno la ufunguzi kutoka kwa Rasi wa Shirikisho la Kikapu Tanzania, Hasheem Thabeet, ambaye pia anatoa taarifa kuhusu ujio wa tuzo za mpira wa kikapu.
Hewani ni Dodoma vs Singida
Ni Basketball Taifa Cup kutoka hapa Chinangali Park, Dodoma.
#TaifaCup2026 #Basketball #Kikapu #BasketballTaifaCup #TBF #DodomaMwanza
- Title
- VITASA | CDF CUP 2026 | Mohamed Mangochi vs Isihaka Shabani | 21/07/2026
- Runtime
- 13:22
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- CDF CUP | Pambano la kwanza limeshuhudia Mohamed Mangochi wa Kamandi ya Makao Makuu (DFHQ) ameshinda kwa pointi dhidi ya isihaka Shabani kutoka Kamandi ya Jeshi la Kujenga Taifa (MMJKT).
Hii ni sehemu tu ya kilichotokea raundi ya tatu nay a mwisho, pambano zima utalipata Youtube.
Ngumi zilikuwa LIVE #AzamSports2HD
#CDFCup2026 #CDFCup #MashindanoYaMkuuWaMajeshi #JeshiLaAkiba #Vitasa #Ngumi #Boxing #MangochiIsihaka
- Title
- VIWANJANI | Maandalizi ya msimu mpya 2026/27 yashika kasi, timu zafanya maboresho ya vikosi vyake.
- Runtime
- 1:02:29
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- MSHIKEMSHIKE 21/07/2026 - AZAMTV
- Runtime
- 50:02
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Azam TV
- Title
- PRESS SIMBA | Wekundu wa Msimbazi watangaza majembe mapya, Simba Day ni Agosti nane
- Runtime
- 1:16:32
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- PRESS SIMBA: “Binadamu wote wataanza kutembea kinyumenyume”
Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amesema kuna mchezaji huyo, siku watakapomtambulisha, dunia itabadilisha tabia yake ya sili na hapo ndipo wanapata mashaka ya namna ya kumtambulisha.
Ahmed anasema mchezaji huyo alistahili kuwa Mexico, Canada au Marekani kwenye fainali za Kombe la Dunia ambazo zilimalizika Julai 19, 2026.
Simba imetangaza kwamba Simba Day ya mwaka huu itafanyika Agosti nane na itakuwa katika dimba la Uhuru Dar es Salaam.

