Azam TV
Magoli | Fountain Gate FC 1-2 Pamba Jiji FC | NBC Premier League 30/04/2026.
- Title
- Magoli | Fountain Gate FC 1-2 Pamba Jiji FC | NBC Premier League 30/04/2026.
- Runtime
- 3:47
- Date posted
- 25 days ago
- Description
- #NBCPL Chuma zote tatu hizi hapa, Pamba Jiji wakichukua alama tatu mbele ya Fountain Gate FC.
FT: F/Gate FC 1-2 Pamba Jiji FC
Wafungaji wa Pamba Jiji na Yonta Camara 17' na John Nakibinge 45'+2
Goli la Fountain Gate likifungwa na Chwukunonye Obasi 34'
LIVE #AzamSports1HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi #F/GateFC #PambaJijiFC #FountainPamba
- Title
- SIMBA YATUA DAR | Simba kutangaza viingilio vya Kariakoo Derby ya Mei 3, 2026
- Runtime
- 3:04
- Date posted
- 25 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amewakumbusha wapenda soka kwamba dimba la Meja Jenerali Isamuhyo linaingiza watazamaji wasiozidi 12,000.
Ahmed pia anasema leo watatangaza bei ya viingilio.
Ni kutokea Bandari ya Dar es Slaam, wakati kikosi cha Simba kikiwasili kutokea Zanzibar.
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- SIMBA YATUA DAR | Ahmed Ally alifuta kombe kwa noti ya shilingi 10, 000
- Runtime
- 3:32
- Date posted
- 25 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Tazama ‘mbwembwe’ za Ahmed Ally akilifuta Kombe la Muungano kwa noti ya shilingi 10,000.
Ahmed anasema hakuna muda wa kupoteza na leo hii timu itaingia kambini kwa ajili ya mchezo wa Mei 3, 2026 pale Meja Jenerali Isamuhyo.
Ni kutokea Bandari ya Dar es Slaam, wakati kikosi cha Simba kikiwasili kutokea Zanzibar.
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- SIMBA YAREJEA DAR | Ahmed Allyasema wametoka kwenye minyororo ya kufungwa na Yanga
- Runtime
- 3:01
- Date posted
- 25 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: “Tumefanikiwa kutoka kwenye minyororo ya muda mrefu”
Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally anasema kwa ushindi wa jana Aprili 29, 2026 dhidi ya Yanga SC, umerejesha ukubwa wao na ujasiri wao.
Ni kutokea Bandari ya Dar es Slaam, wakati kikosi cha Simba kikiwasili kutokea Zanzibar.
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Shangwe la mashabiki wa Simba bandarini wakati wakirejea Dar es Salaam na kombe lao
- Runtime
- 0:48
- Date posted
- 25 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Tazama shangwe la mashabiki wa Simba SC, wakishangilia baada ya kurejea Dar es Salaam, wakitokea Zanzibar ambako walitwaa taji la #MuunganoCup2026 kwa kuifunga Yanga SC goli 1-0 jana Aprili 29, 2026.
Ni kutokea Bandari ya Dar es Slaam, wakati kikosi cha Simba kikiwasili kutokea Zanzibar.
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Simba yatua Dar kwa kishindo, wenyewe wasema sherehe zimeisha na sasa wanawaza Mei 3, 2026
- Runtime
- 2:38
- Date posted
- 25 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: “Mechi ya Simba na Yanga haijawahi kuwa nyepesi”
Mratibu wa Simba SC, Abbas Ally anasema watani wao wa Yanga SC, walikuwa wanaamini mchezo wa fainali ungekuwa mwepesi, lakini kiuhalisia #KariakooDerby haijawahi kuwa nyepesi.
Abbas anasema sherehe shimekwisha na sasa ni maandalizi kuelekea Mei 3, 2026 katika dimba la Meja Jenerali Isamuhyo.
Ni mahojiano ya yaliyofanyika kutoka Bandari ya Dar es Slaam, wakati kikosi cha Simba kikiwasili kutokea Zanzibar.
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Ahmed Ally atoa neno baada ya Derby ya Kariakoo.
- Runtime
- 1:48
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: “Tumefanikiwa kuvunja uteja”
Sehemu ya maneno ya Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally baada ya kubeba taji la Muungano Cup 2026.
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
Ilikuwa LIVE #AzamSports1HD
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Seleman Mwalimu na Nickson Kibabage
- Runtime
- 2:41
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Mshambuliaji wa Simba, Selemani Mwalimu na beki Nickson Kibabage watoa neno baada ya mechi.
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
Ilikuwa LIVE #AzamSports1HD
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- MUUNGANO CUP 2026 | Kocha Steve Barker aipongeza Yanga - 29/04/2026
- Runtime
- 1:38
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: “Young Africans ni timu nzuri”
Kocha wa Simba SC, Steve Barker anasema mechi ilikuwa ngumu huku akiwapongeza wachezaji wake kwa namna walivyopambana.
Kocha huyo ameonesha kufurahishwa na kiwango cha Selemani Mwalimu.
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Yanga SC 0-1 Simba SC | Highlights Muungano Cup 2026 - 29/04/2026
- Runtime
- 15:09
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa fainali ya Muungano Cup 2026 kati ya Yaanga SC dhidi ya Simba SC.
Simba imenyakua taji kwa goli la penati la Selemani Mwalimu.
FT: Yanga 0-1 Simba SC
- Title
- MUUNGANO CUP 2026 | Simba yakabidhiwa taji la Muungano Cup 2026 - 29/04/2026
- Runtime
- 2:53
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Shangwe la Simba SC, baada ya kukabidhiwa taji la #MuunganoCup2026
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- MUUNGANO CUP 2026 | Simba yakomba tuzo za mashindano ya Muungano Cup - 29/04/2026
- Runtime
- 3:52
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Kocha Bora ni Steve Barker, Hussein Mbegu ni Mchezaji Bora kijana, Selemani Mwalimu ndiye Mfungaji Bora huku Rushine De Reuck akiwa ndiye Mchezaji Bora wa Mashindano.
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Goli kwa lugha ya Kiingereza | Yanga SC 0-1 Simba SC | Muungano Cup 2026 - 29/04/2026
- Runtime
- 2:07
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Msikie mtangazaji Peter Otai alivyosherehesha goli la Simba kwa lugha ya Kiingereza.
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Yanga SC 0-1 Simba SC | Goli | Muungano Cup 2026 - 29/04/2026
- Runtime
- 2:05
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: Hili hapa goli la Simba SC likifungwa na Selemani Mwalimu kwa mkwaju wa penati.
Ni Clatous Chota Chama ambaye alifanya ufundi mbele ya Edmund John, na kusababisha penati kisha Mwalimu akaweka golini akimpoteza Djigui Diarra.
AET: Yanga SC 0-1 Simba SC
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- Azam FC TV | 28 |2026 | Kikosi cha Azam FC kilivyotalii ndani ya Zanzibar
- Runtime
- 23:21
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- KARIAKOO DERBY | Tuvituvitu vya mechi ya Yanga dhidi ya Simba
- Runtime
- 0:44
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCupFinal: ‘Tuvituvitu’ vya dabi.
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSimba
- Title
- KARIAKOO DERBY | Muro afunguka upekee wa mechi ya fainali ya Yanga Vs Simba
- Runtime
- 2:30
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCup2026: Mtaalamu wa soka @godlisten_muro7 anafunguka upekee wa mchezo wa leo kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC.
Fainali ni Yanga vs Simba , leo Aprili 29, 2026.
#MuunganoCup2026 #KombeLaMuungano #SokaLinatuunganisha #NyerereKarumeDay
- Title
- Kariakoo Derby | Mchambuzi wa soka Ramadhan Mbwaduke anafunguka utamu wa dabi
- Runtime
- 1:41
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCup2026: Mchambuzi wa soka Ramadhan Mbwaduke anafunguka utamu wa mechi ya leo ya fainali ya #MuunganoCup2026.
Mbwaduke anasema Yanga inahitaji kulitetea taji huku Simba ikihitaji kuanza kuchukua makombe ambayo hivi karibuni imekuwa ikiyakosa.
Fainali ni Yanga vs Simba , leo Aprili 29, 2026.
#MuunganoCup2026 #KombeLaMuungano #SokaLinatuunganisha #NyerereKarumeDay
- Title
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI | UFM Radio yasema heshima haiombwi kwa maneno, Kamwe, Ahmed watamba
- Runtime
- 11:13
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- ZILIZOBAMBA MITANDAONI: UFM Radio wanasema heshima haiombwi kwa maneno.
Ni kuelekea mchezo wa leo wa ‘Dabi’ ya Kariakoo kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC.
Kamwe asema Zanzibar imechangamka baada yay eye kufika, Ahmed asema wapo tayari.
Ni Zilizobamba mitandaoni ya #Viwanjani
#Viwanjani
- Title
- VIWANJANI : Fainali ya Kombe la Muungano kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC ni leo Aprili 29, 2026
- Runtime
- 58:48
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- Wachambuzi wa soka,Lilian Mukulu na Adriano James wakitoa mitazamo yao kuhusu mchezo wa fainali ya Kombe la Muungano unaozikutanisha Yanga SC dhidi ya Simba SC.
Adriano amesema taswira nzima inakupa picha ya mchezo mgumu kutokana na uimara wa wachezaji wa pande zote mbili.
Kwa upande wake Mukulu amesema fainali hii ni mchezo ambao kila mpenda soka anaisubiri kwa hamu kuona kile wachezaji wa pande zote mbili wataonesha uwanjani.
Mchezo ni leo Aprili 29,2026 saa 2:15 na utakuwa LIVE #AzamSports1HD
- Title
- Ujue utofauti wa Amaan Stadium na New Amaan Complex
- Runtime
- 6:50
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCup2026: Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF), Hussein Ahmada Vuai, ametoa ufafanuzi kuhusu utofauti wa New Amaan Complex na Amaan Stadium.
Vuai anasema New Amaan Complex, inahusisha vitu kadhaa ikiwemo viwanja viwili vya mazoezi pamoja na hoteli.
Lakini Amaan Stadium ni ule uwanja unaotumika kuchezea mechi.
Leo Aprili 29, 2026, saa 2:15 usiku itapigwa fainali ya #MuunganoCup2026 na itakuwa LIVE #AzamSports1HD
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSC #SimbaSC
- Title
- Baraka Mpenja kutoka Zanzibar
- Runtime
- 3:14
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- #MuunganoCup2026: Mtangazaji wa mechi ya leo kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC kwenye fainali ya #MuunganoCup2026 ‘Sauti ya Radi’ Baraka Mpenja anasimulia ‘kituko’ kilichotokea jana Aprili 28, 2026 wakati Simba na Yanga zilipokuwa mazoezini katika viwanja vilivyopo ndani ya viunga vya New Amaan Complex, Zanzibar.
Mpenja anasema katika mazoezi hayo ya mwisho ambayo timu zote mbili zilifanya muda mmoja, kila timu ilijaribu kurusha ndege nyuki (drone) kuielekeza kwa mwenzake kiasi ambacho zilikaribia kugongana angani.
Mtanange ni leo Aprili 29, 2026, saa 2:15 usiku na itakuwa LIVE #AzamSports1HD
#MuunganoCup2026 #KariakooDerby #YangaSC #SimbaSC
- Title
- KARIAKOO DERBY | Vita ya maneno ya mashabiki wa Simba na Yanga
- Runtime
- 6:26
- Date posted
- 26 days ago
- Description
- KUTOKA MTWARA: Mashabiki wa Simba SC na Yanga SC watambiana kuelekea mchezo wa fainali ya #MuunganoCup2026.
Mashabiki wa Yanga SC wamesema wataendeleza ubabe mbele ya mtani wao Simba SC huku wakijivunia uwepo wa kiungo wao Allan Okelo.
Kwa upande wa mashabiki wa Simba SC wametamba timu yao kuibuka na ushindi kutokana na ubora wa wachezaji wao.
Mchezo ni leo Aprili 29,2026 saa 2:15 na utakuwa LIVE #AzamSports1HD
viwanjani
- Title
- MAKALA | Maajabu ya Wonder Kids kwenye kukuza vipaji vya soka, Kocha Zahera ndiye mshika bendera
- Runtime
- 1:19:53
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- MSHIKEMSHIKE | 28 /04/2026
- Runtime
- 44:42
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- Azam TV
- Title
- Benjamin Mkapa yaanza kurekebishwa ili kukidhi matakwa ya CAF
- Runtime
- 2:53
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- BENJAMIN MKAPA: “Tumeweka kampuni kubwa na yenye sifa za kimataifa”
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, anasema kazi ya marekebisha ya Uwanja wa Benjamin Mkapa imeanza na tabaka la juu la sehemu ya kuchezea, itaondoshwa yote na kuwekwa tabaka jipya ili maji yasiweze kutuama.
#BenjaminMkapa #Stadium
- Title
- Baruan Muhuza, Kocha mkwasa, wasanii wa sauti wamwelezea marehemu Hashim Kambi
- Runtime
- 2:39
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- BURIAN HASHIM KAMBI: “Umri wake mkubwa lakini bado alibaki kuwa maridadi sana”
Meneja Mwandamizi wa #AzamMedia ambaye pia ni mkuu wa @ufmradiotz Baruani Muhuza anasema miongoni mwa sifa za marehemu Hashim Kambi ni ucheshi aliodumu nao nyakati zote.
Baruani anasema uso wa Mzee Kambi ulitawaliwa na tabasamu muda wote.
Kocha Boniface Mkwasa anasema Mzee Kambi alikuwa anaweza kucheza nafasi zote za mstari wa nyuma kama vile namba sita, namba tano na nne enzi hizo akisakata ‘kabumbu’
Kwa upande wake mnakilisha sauti Chausiku Lukinga, anasema yeye ndiye aliyempisha studio ilipofika zamu yake jana Aprili 27, 2026.
Msanii huyo wa filamu na mchezaji wa zamani wa Yanga SC, alifariki dunia jana Aprili 27, 2026.
#RIPKambi
- Title
- Wakongwe Simba, Yanga watoa neno fainali ya Muungano Cup 2026
- Runtime
- 2:28
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- DABI YA KARIAKOO: “Dabi haina mwenyewe”
Nyota wa zamani wa Simba SC, Thomas Kipese anasema ni vigumu kuizungumzia kwa undani mechi inayohusisha Simba na Yanga.
Kipese anasema unaweza kuamini Simba ipo vizuri, lakini mshindi akawa Yanga na waweza kuhisi Yanga yupo vema, lakini Simba ndio ikashinda.
Mohamed Kampira, Seleman Kaburu na Kaingilila Maufi nao wametoa neno kuhusu mechi hiyo.
Ni kuelekea mechi ya fainali ya #MuunganoCup2026 ambayo itachezwa kesho Jumatano Aprili 29, 2026, kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC.
Mechi ni saa 2:15 usiku na itakuwa LIVE #AzamSports1HD
#MuunganoCup2026 #Yanga #Simba
- Title
- Bondia Ibrahim Class afichua siri ya ushindi wake nchini Thailand
- Runtime
- 4:20
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- MAPOKEZI YA BONDIA IBRAH CLASSIC: “Kazi yangu ilikuwa ni kula na kufanya mazoezi”
Bondia Ibrahim Class amewashukuru wale wote waliomshika mkono katika nyakati ambazo alikuwa kwenye kambi kwa ajili ya pambano lake lililofanyika Aprili 24, 2026, jijini Bangkok Thailand.
Bondia huyo ametua leo kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam baada ya kushinda Ubingwa wa Kimataifa Mkanda wa WBC katika uzani wa kilo 59.
Bondia huyo amewasili leo Aprili 28, 2026, saa nane mchana.
Tulikuwa LIVE #AzamSports3HD
#Vitasa #MfalmeWaNgumi
- Title
- Mapokezi ya Ibrahim Class Uwanja wa Ndege Dar es Salaam
- Runtime
- 1:59
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- MAPOKEZI YA BONDIA IBRAH CLASSIC: Tazama shangwe la mashabiki wa ngumi waliojitokeza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, kumpokea bondia Ibrahim Class, ambaye ameshinda Ubingwa wa Kimataifa Mkanda wa WBC katika uzani wa kilo 59.
Pambano hilo lilifanyika Aprili 24, 2026 jijini Bangkok, Thailand.
Bondia huyo amewasili leo Aprili 28, 2026, saa nane mchana.
- Title
- PIN POINT | Maeneo ambayo Simba SC inapaswa kurekebisha kabla ya kuivaa Yanga
- Runtime
- 1:17
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- PIN POINT: ‘Mwamba wa Juu’ @leomusikula_tz leo anawakumbusha magolikipa wa Simba SC na mabeki kuzingatia mambo ambayo yanaweza yakawasababishia madhara kwenye mechi ya #MuunganoCup2026 na mashindano mengine.
Musikula ameangazia kosa alilowahi kufanya golikipa Mahamadou Kasali kwenye #MzizimaDerby iliyopigwa katika dimba la Azam Complex, japo halikuleta madhara kwa upande wao.
Na kosa lingine lilitokea kwenye mechi ya #MuunganoCup2026 dhidi ya Mlandege ambapo golini alikuwa Hussein Abel, japo na hapo pia mnyama alitoka salama.
#PinPoint
- Title
- VIWANJANI : Kariakoo Derby kutimua vumbi kesho kwenye mashindano ya muungano.
- Runtime
- 36:14
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- Iddy Nonga na Andrew Kingamkono wakitoa maoni yao kuhusu mchezo wa kesho kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC.
Nonga anasema vikosi vya timu zote vinaonekana kuwa tayari kwa mchezo huo hivyo tutegemee burudani ya soka.
Kwa upande wake Kingamkono anasema timu ya Yanga SC kwa sasa wachezaji wake wamezoeana na kuwa hatari zaidi mbele ya lango la wapinzani.
- Title
- VIWANJANI : Mashabiki wa Simba SC na Yanga SC , Iringa watambiana kufungana.
- Runtime
- 6:11
- Date posted
- 27 days ago
- Description
- Kuelekea kwenye mchezo wa Kariakoo Derby katika mashindano ya muungano utakaochezwa kesho Aprili 29, katika dimba la New Amaan, Zanzibar.
Mashabiki wa timu hizo kutoka mkoani Iringa wametamba timu zao kufanya vema.
- Title
- MSHIKEMSHIKE - AZAM TV 27/04/2026
- Runtime
- 45:30
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Tazama kipindi cha Mshikemshike kikiwa na habari mbalimbali za michezo ikiwemo maandalizi ya Kariakoo Derby kwa ajili ya fainali ya Muungano Cup na mechi ya NBC Premier League.
- Title
- BURIANI MZEE KAMBI | Aliwahi kukumbushia namna alivyoiokoa Yanga kufungwa na Simba
- Runtime
- 2:40
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- BURIANI MZEE KAMBI: “Sisi tulikuta Yanga ikiwa mtumwa wa watani wetu Simba”
Maneno ya msanii wa filamu nchini marehemu Hashim Kambi alipokumbushia moja ya mambo ambayo hawezi kuyasahau wakati akicheza Yanga SC.
Mzee Kambi ambaye amefariki dunia leo Jumatatu Aprili 27, 2026, aliwahi kusema kuwa alitoa pasi ya goli mwaka 1980 na kuiokoa Yanga kutoka kwenye kufungwa kwa muda mrefu.
#RIPKambi #HashimKambi
- Title
- KARIAKOO DERBY | Ahmed Ally asema hakuna anayependa mechi ya dabi
- Runtime
- 4:44
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- MUUNGANO CUP 2026: “Tumehamasika kwa kiasi kikubwa”
Nyota wa Simba SC, Neo Maema anasema #KariakooDerby ni moja michezo yenye hadhi ya juu Afrika Mashariki na kushinda ni jambo zuri.
Kwa upande wake Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally anasema kikosi chao kimeanza rasmi mazoezi leo na kimsingi dabi ni mechi ambayo hakuna timu inaweza kujitokeza ikasema ina uhakika wa kushinda.
Ahmed anasema hakuna mtu ambaye huipenda mechi ya dabi kwasababu matokeo ya aina yoyote ya matokeo huleta hekaheka kwa timu zote mbili.
Mechi ni Aprili 29, 2026, saa 2:15 usiku LIVE #AzamSports1HD
#KariakooDerby #Yanga #Simba
- Title
- Mwamnyeto, Walter Harson wafunguka kuhusu Dabi ya Kariakoo
- Runtime
- 2:53
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- MUUNGANO CUP 2026: “Fainali imekuwa ya kipekee”
Meneja wa Yanga SC, Walter Harson, anasema mashabiki wa Yanga SC, wanasubiri taji la Muungano Cup na wao wapo tayari kulitetea taji hilo.
Kwa upande wake nahodha Bakari Mwamnyeto anasema wao wapo kamili kuwakabili wapinzani Simba na kuwaomba mashabiki wajitokeze wengi kuwapa nguvu.
Mechi ni Aprili 29, 2026, saa 2:15 usiku LIVE #AzamSports1HD
#KariakooDerby #Yanga #Simba
- Title
- PIN POINTI | Mchambuzi ataka kujua anayesema Chama hana kasi akiwa uwanjani
- Runtime
- 1:34
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- PIN POINT: Nani amekwambia Chama hana kasi…..???????
Ni swali ambalo anauliza ‘Mwamba wa Juu’ @leomusikula_tz kuhusu yale anayofanya Clatous Chota Chama hasa kwenye michuano ya Muungano Cup 2026.
Katika mchezo wa jana Aprili 26, 2026, dhidi ya Mlandege, Chama alitoa pasi mbili zilizozaa magoli.
Jumatano ni ‘Dabi ya Kariakoo’ katika mashindano ya Muungano Cup 2026.
Moto wa Chama utakuwaje…???
#PinPoint
- Title
- VIWANJANI : Timuatimua ya makocha kwa baadhi ya timu NBC Premier League.
- Runtime
- 25:39
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Wachambuzi wa soka Godlisen Muro na Andrew Kingamkono wanakudadavulia kwa kina sababu mojawapo zinazochangia klabu nyingi kuvunja mikataba na makocha NBC Premier League.
- Title
- VIWANJANI: Historia inaenda kuandikwa, Derby ya Kariakoo kuchezwa mara mbili ndani ya wiki moja.
- Runtime
- 14:55
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Andrew Kingamkono na Godlisen Muro wanakupitisha kwenye uchambuzi murua kuhusu Derby ya Kariakoo ndani ya mashindano ya Muungano na Kwenye NBC Premier League.
#viwanjani
- Title
- PIN POINT| Ushirikiano wa Damaro, Okello, Dube pale Yanga, waumiza kichwa wapinzani
- Runtime
- 1:34
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- PIN POINT: Ebana leo ‘Mwamba wa Juu’ Leonard Musikula anaangazia ‘combo’ ya wachezaji watatu wa Yanga SC, namna wanavyoshirikiana kwenye kutengeneza magoli hasa katika mashindano ya Muungano Cup.
Ni Mohamed Damaro Camara, Allan Okelo na Prince Dube. Watatu hao wameonesha ushirikiano wao kwenye mechi dhidi ya Muembe Makumbi na Azam FC.
Tazama namna combo yao inavyotengeneza magoli.
#PinPoint
- Title
- VIWANJANI : Uchambuzi Yanga SC na Simba SC zilivyofuzu hatua ya nusu fainali Muungano Cup.
- Runtime
- 36:41
- Date posted
- 28 days ago
- Description
- Wachambuzi Godlisen Muro na Andrew Kingamkono wakieleza maoni yao kuhusu michezo miwili ya nusu fainali Muungano Cup.
Muro amesema kitu kilichoua mechi ya Yanga SC dhidi ya Azam FC ni uhatari wa Yanga bila ya kuwa na mpira, walikuwa wepesi sana kwenye kupokonya mpira na kukimbia kwa haraka zaidi, jambo lilisababisha Azam kufanya makosa mengi zaidi kwenye eneo la ulinzi.
- Title
- Mlandege FC 0-3 Simba SC | Highlights | Muungano Cup 2026 - 26/04/2026
- Runtime
- 11:24
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mechi kati ya Simba SC dhidi ya Mlandege FC.
Simba imeshinda magoli 3-0
Wafungaji ni Seleman Mwalimu, Anicet Oura na Neo Maema.
- Title
- Mlandege FC 0-3 Simba SC | Magoli | Muungano Cup 2026 - 26/04/2026
- Runtime
- 3:21
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- Tazama magoli yote matatu ya Simba SC ikiichapa Mlandege FC.
Simba imeshinda magoli 3-0
Wafungaji ni Seleman Mwalimu, Anicet Oura na Neo Maema.
- Title
- MASHEMEJI DERBY | AFC Leopards 0-1 Gor Mahia | Goli | Sport Pesa League - 26/04/2026
- Runtime
- 1:39
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- #SportPesaLeague: Chuma hii hapa ikiwekwa nyavuni na Alpha Onyango akiipatia Gor Mahia alama tatu muhimu.
FT: AFC Leopards 0-1 Gor Mahia
#LigiKuuKenya #SportPesaLeague #AFCLeopards #GorMahiaFC
- Title
- Simba Queens 1-0 Ceassiaa Queens | Goli | Ligi Kuu ya Wanawake - 26/04/2026
- Runtime
- 1:28
- Date posted
- 29 days ago
- Description
- #TWPL: ‘Chuma’ hii hapa ya Fasila Odhiambo akiipatia Simba Queens goli la pointi tatu.
FT: Simba Queens 1-0 Ceassiaa Queens
#TWPL #WPL #TanzaniaWomenPremierLeague #LigiKuuWanawake #LigiYaWanawake #WomenFootball #WomenPremierLeague #SimbaQueensVsCeassiaaqueens
- Title
- Azam FC 1-2 Yanga SC | Highlights Muungano Cup 2026 - 25/04/2026
- Runtime
- 12:50
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa nusu fainali ya Muungano Cup kati ya Azam FC dhidi ya Yanga SC.
Yanga imeshinda kwa jumla ya magoli 2-1.
Magoli ya Yanga yamefungwa na Prince Dube na Maxi Nzengeli.
Goli la Azam FC mfungaji ni Feisal Salum.
- Title
- Azam FC 1-2 Yanga SC | Magoli | Muungano Cup 2026 - 25/04/ 2026
- Runtime
- 2:53
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Tazama magoli yote matatu yaliyofungwa kwenye mchezo wa nusu fainali ya Muungano Cup 2026 kati ya Azam FC dhidi ya Yanga SC.
Magoli ya Yanga yamefungwa na Prince Dube na Maxi Nzengeli.
Goli la Azam FC limefungwa na Feisal Salum.
- Title
- Afisa Masoko wa AzamPesa, Edward Alex ametoa elimu kwa umma kuhusu matumizi ya huduma ya Azam Pesa.
- Runtime
- 12:11
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Afisa Masoko wa AzamPesa, Edward Alex, ametoa elimu kwa umma kuhusu matumizi ya huduma ya Azam Pesa, akieleza manufaa na urahisi wa kuitumia katika shughuli za kila siku za kifedha.
Akizungumza jana katika kipindi cha Viwanjani, Edward amesema huduma hiyo imeboreshwa ili kurahisisha miamala mbalimbali, ikiwemo kutuma na kupokea fedha kwa haraka, salama na kwa ufanisi zaidi.
Ameongeza kuwa Azam Pesa inalenga kuwapa watumiaji suluhisho la kisasa la kifedha linalowawezesha kufanya miamala kwa urahisi, huku ikihakikisha usalama wa fedha zao wakati wote.
- Title
- YANGA TV 25/04/2026 | Kufungwa mchakato mzima wa mchujo wa kwanza Yanga soka school.
- Runtime
- 25:22
- Date posted
- 1 month ago
- Description
- Yanga TV wiki hii inakuletea taarifa ya kina kuhusu kufungwa rasmi kwa mchakato wa mchujo wa watoto 30 watakaopata mafunzo ya soka kupitia program ya Yanga soka school.
Pia ilikuwa ni wiki ya mchezo wa kwanza kwenye mashindano ya Muungano Cup dhidi ya Muembe Makumbi FC.

